Jumatano, 10 Mei 2017

MOYO WA MTU HUAMBATANA NA MUNGU AU MALI.

MOYO WAKO UMEAMBATANA NA MUNGU AU MALI

HALELUYA

Mathayo 19;16~24

16 Na tazama mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu nitende jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?
17 Kwani kuniuliza habari ya wema? Alieye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima zishike amri
18 Akamwambia zipi? Yesu akasema, Ni hizi usiue,usizini,usiibe,usishuhudie uongo,
19 Waheshimu baba yako na mama yako na mpende jirani yako kama nafsi yako.
20 Yule kijana akamwambia, haya yote nimeyashika nimepungukiwa na nini tena?
21 Yesu akamwambia ukitaka kuwa mkamilifu enenda ukauze ulivyo navyo uwape masikini nawe utakuwa na hazina mbinguni kisha njoo unifuate
22 Yule kijana alipo sikia neno lile akaenda zake kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Yesu akawaambia wanafunzi wake amini nawaambieni ya kwamba itakuwa shida tajili kuingia katika ufalme wa Mbinguni
24 *Nawaambia tena ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu*

Bwana Yesu apewe sifa sana

Tumesoma habari ya yule kijana tajiri anamuuliza Yesu kwamba afanye nn aulithi ufalme wa mbinguni. Kijana alipenda kwenda mbinguni na ndio maana anamuuliza Yesu kwamba afanye nn ili aingie mbinguni Yesu anamuuliza kama anazijua amri kijana alimjibu kuwa yote ameyashika na anayafanya sasa kwa kuwa alikuwa na shauku ya kutaka kuingia mbinguni anamuuliza nimepungukiwa nn tena kama ni amri anazijua na anayafanya ingekuwa ni mtu mwingine ingewezekana kwa kuwa Yesu amemwambia amri na anazijua angeishia hapo kuuliza angesha jua mbingu yangu lkn kijana akawa na shauku ili ajua labda kama amepungukiwa kitu kisimfanye aende mbinguni na Yesu ndipo anamjibu na Yesu aliijua shauku ya kijana na aliona kabisa huyu anapenda kwenda mbinguni na alijua pamoja na kijana kutaka kwenda mbinguni yulr kijana moyo wake ulikuwa haujashikamana na nae ila umeshikamana na mali ndipo anamwambia kauze vyote ulivyo navyo ukawape maskin kisha unifuate. Kijana aliondoka kwa huzuni sababu moyo wake ulikuwa kwenye mali na sio Mungu na ndio maana jibu la Yesu lilimfadhaisha sana. Ni kweli kijana alitaka kwenda mbingun lkn moyo haukuwa na Mungu bali mali
Yesu alipo kuwa anamwambia kijana akauze mali zake hakuwa na maana amfilisi ila alitaka kujua kama kweli moyo wake umeshikamana naye

Mpendwa Mungu anapo tuambia tumtolee sadaka si kwamba amataka pesa zetu sababu vyote ni mali yake anataka kupima mioyo yetu kama kweli tunampenda Mungu na kujitoa hata kwa mali kwa ajili yake. Na ndio maana anasema tutoe kwa hiyari yaan mioyo ya kupenda lkn pia maandiko yanasema hazina na mtu ilipo na moyo wake ulipo inamaana ww ukitoa kasehemu kadogo ka mali zako ndio kaupendo kako kalivyo kwa Mungu

Hebu tusome mf huu kwa baba yetu Ibrahimu tuone jinsi sadaka ilivyo na nguvu na Mungu jinsi anavyo tupima

Mwanzo 22;1~12
Hapa tunasoma habari za Ibrahimu. Mungu alimjaribu akamwambia amtoe sadaka mwanae wa pekee si kwamba Mungu alikuwa akimtaka Isaka na si kwamba Mungu alikuwa hajui kama Ibraimu hamchi yeye ila alimjaribu kuupima moyo wake kama kweli Ibrahimu anampenda Mungu kwa moyo wake na Mungu alithibitisha hilo kwamba kweli.Ibrahimu anampenda kwa maana hakumzuilia mwanae wa pekee alitaka kumchinja soma mstr wa 12

Hivyo mpendwa Mungu akikusemesha kwa habar ya kutoa hata kiwe kitu muhimu vip kwako toa sababu Mungu haitaji hicho anahitaji ule utayari wako wa kujitoa kwa moyo kwa ajili yako.

Je moyo wako.umeshikamana na nani Mungu au mali au kazi kama ni Mungu jipime unavyo jitoa kwa ajili ya Mungu ile kwa mali au muda hicho ndicho kitakacho kuthibitishia unampenda Mungu hebu muangalie mama mjane alitoa senti mbili lkn Yesu alimuona ametoa kuliko wote sababu hakutoa sehemu ya mali bali alitoa kwa moyo tena chote alicho nacho Mungu.anaangalia moyo wako unavyo jitoa angalii kiasi unachotoa na moyo ndio kipimo cha ww unampenda Mungu

kijana alishindwa kuendelea na Yesu sababu alikuwa na mali nyingi sana na moyo wake ulikuwa kwenye mali alizo nazo sio kwa Yesu

Je ww moyo wako uko wapi?
Je unampenda Mungu kweli?
Je unajitoa kiasi gani kwa ajili ya Mungu

Ibrahimu Mungu alipo uona moyo wake kwamba anamcha Mungu akumzuilia mwana wake wa pekee Mungu alimbariki Ibrahimu alitengeneza agano nae mpaka leo watu tujajibarikia katika uzao wake taifa la Israeli

SADAKA YAKO IAMBATANE NA MOYO WAKO NA MOYO WAKO UAMBATANE NA BWANA SI MALI.

Amosi 3;3 je! watu wawili waweza kutembea pamoja wasipokuwa wamepatana?
Hauwezi kutembea na mtu pasipo kupatana naye. Namaanisha Huwezi kutembea na Mungu au kuwa karibu na Mungu wakati moyo wako upo mbali nae na moyo wako kuwa karibu nae ni vile unavyo jitoa kwa ajili yake(MUNGU)  na kutembea katika sheria zake.

ROHO MTAKATIFU aendelee kukufundisha.

Barikiwa .

Jumanne, 2 Mei 2017

JE, YESU KRISTO NA MUHAMMAD WALITUMWA NA MUNGU MMOJA?

Kumekuwa na hoja moja ambayo inasumbua vichwa vya watu wengi.
Je, YESU NA MUHAMMADCWALITUMWA NA MUNGU MMOJA?
Leo nakata utepe kwa kutumia BIBLIA na Quran. Tunapaswa kuangalia hoja moja ya msingi, je kauli zao zinafanana? au zinapingana? Kama hazifanani yakupasa ujiulize mara mbili mbili, kati ya Moja na Mbili ipi iliabza kujitambulisha na ipi ilikanusha utambulisho.
Muhammad alizaliwa mwaka 570 bk,
Wakati anazaliwa aliikuta kauli hii
Mathayo : Mlango 3
17 na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.
Pia andiko hili alilikuta, ambalo ni KAULI YA MALAIKA
Luka : Mlango 1
32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
Hoja ya msingi ni kwamba, Je Malaika aliyetumwa na Mungu kusema kauli hii, ndiye aliyetumwa tena kupinga kauli tangulizi?
Lazima tujiulize kuhusu hili.
Tazama Quran 2:116
116.
Na ati wanasema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu! Ametakasika na hayo. Bali vyote viliomo mbinguni na duniani ni vyake. Vyote vinamt'ii Yeye.
Hii kauli ilikuja kupinga kauli inayopatikana kwenye LUKA 1:30-37
Ambayo inasema

Luka 1:
30. Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.
34 Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?
35 Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.
36 Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa;
37 kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.



Watu wote Wanajua kuwa MUNGU hawezi kujipinga atamkapo.

Hapo tu unapata picha kuwa, Wawili hawa walitoa ujumbe sehemu mbili tofauti.

Ukisoma Biblia iliyotangulia kuleta huu ujumbe juu ya YESU KUITWA MWANA WA MUNGU miaka 600 kabla ya kushuka aya zilizo kanusha ujumbe wa mwanzo.


Hapa yatupasa kuwa makini.


Tazama Quran 4:171


171.
Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu, wala msimseme Mwenyezi Mungu ila kwa lilio kweli. Hakika Masihi Isa mwana wa Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na neno lake tu alilo mpelekea Maryamu, na ni roho iliyo toka kwake. Basi Muaminini Mwenyezi Mungu na Mitume wake. Wala msiseme: Utatu. Komeni! Itakuwa kheri kwenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja tu. Ametukuka Yeye na kuwa na mwana. Ni vyake Yeye vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mtegemewa wa kutosha.

Hii aya inapinga Maneno ya YESU yanayopatikana katika 

 YOHANA 9:35-37 inasema hivi


35 Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu?
36 Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini?
37 Yesu akamwambia, Umemwona, naye anayesema nawe ndiye.
38 Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia.
39 Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.


Hapa kuna habari kuhusu vipofu wa kiroho, ambapo YESU anathibitisha kuwa ANAPASWA KUAMINIWA KUWA NDIYE MWANA WA MUNGU.

Kumbuka aya zinasema kuwa YESU HAKUFANYA DHAMBI HATA SIKU MOJA, 

Hivyo  kitendo cha Muhammad kusema kuwa YESU SI MWANA WA MUNGU NI Kumaanishi kuwa YESU ni mwongo baada ya kujiita MWANA WA MUNGU.



Na kama 
ni hivyo inamjumlisha na MALAIKA aliyrtumwa na MUNGU, pia MUNGU aliyemtuma MALAIKA + YESU WOTE NI WAONGO, HILI HALIKUBARIKI. Maana Aya zinasema YESU hakutenda dhambi na ujumbe wake hauwezi kuwa wa UONGO bali KWELI YAKE INABAKI KUWA KWELI MILELE YOTE.




Kwa mujibu wa Quran inaonyesha kuwa mwongo kwa kujiita MWANA WA MUNGU.
Hapa unapata jibu kuwa YESU na Muhammad walitumw na Miungu tofauti kulingana na maneno yao.


YESU ALIKIRI KWA KINYWA CHAKA PALE ALISEMA


YESU alisema anapaa kwenda kwa Baba yake, ambaye ni Mungu wake pia ni Baba yetu, pia Mungu wetu.



HUYU MUNGU ALIYE MTUMA YESU YEYE NI BABA WA WOTE,


Ila huyu aliyemtuma Muhammad hakubaliani na jambo hili na anadai kuwa inakaribia mbingu na ardhi kutatuka kisa Kuitwa Baba, yaana ukisema kuwa YESU ni Mwana wa Allah umeleta mtafaruku mkubwa.

Kwa ushahidi soma aya hii kutoka kwenye Quran 👇👇

Quran 19:

88.
Na wao ati husema kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana!
89.
Hakika mmeleta jambo la kuchusha mno!
90.
Zinakaribia mbingu kutatuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande.
91.
Kwa kudai kwao kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana.
92.
Wala hahitajii Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa na mwana


.
Quran 6 : 101 Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi. Inamkinikaje Awe na mwana, hali Hana mke. Naye ndiye aliyeumba kila kitu (siyo baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu.

Inakuwa mjuzi wa kila kitu au muweza wa vyote ASHINDWE NA KITU KIMOJA TU!!! YAANA KUTO KUWA NA MWA A eti mpaka awe na mke?


Hapa unapata picha kuwa walitumwa na Miungu tofauti. Huhitaji kuvaa miwani ili ulione vizuri au ulielewe vyema.

👇👇👇👇
Quran 18:4-5


4. Na kiwaonye wale wanaosema Mwenyezi Mungu amejifanyia mtoto.

5. Wao hawana ilimu juu ya (jambo) hili wala baba zao ( hawana ujuzi juu ya jambo hili ilawanajisemea tu). Ni neno kubwa hilolitokalo katika vinywa vyao. Hawasemi ila uwongo tu.


Hapo ndio tupate kujua mbivu na mbichi.

Inamaana kuwa YESU ALIPOJIITA MWANA WA MUNG, alikosea na quran imekuja kupitia Muhammad imekuja kumuonya mtu ambaye hana kosa wala hakuwahi kutenda dhambi.


Kwa kauli ya Allah ya Muhammad mtume wake tunapata jibu kuwa YESU ni mwenye dhambi?

Haitokuwa hata siku kupata kosa la Yesu ila kujilisha upepo tu kewa Muhammad na mungu wake Allah.


Sasa twende kwenye utata huu ni kweli aliyejiita MWANA WA MUNGU ( ikaonekana ni kosa )  baadae aitwe MWENYE HEAHIMA MBINGUNI NA DUNIANI?

Quran 3:39

39. Mara Malaika akamlingania, hali amesima akisali chumbani, kwamba Mwenyezi Mungu anakupa khabari njema za (kuwa utazaa mtoto; umwite Yahya, atakaye kuwa mwenye kumsadikisha (Mtume atakayezaliwa)  kwa Nenolitokalo kwa Mwenyezi Mungu (Naye ni Nabii Isa) na  atakayekuwa Bwana kabisa na mtawa na nabii anayetokana na watu wema. (Naye ni nyinyi)


Aya hii inahusu kuzaliwa kwa YOHANA NA YESU. 


Kwanza Yohana atazaliwa na atatabiri kuhusu Ujio wa Yesu, na ya kuwa Yesu atakuwa Bwana.
Tafsiri ya BARWAN inasema MHEAHIMIWA MBINGUNI NA AKHERA.


Ni kweli huyu ATAKAYEKUWA MHESHIMIWA ndiye aliyejiita MWANA WA MUNGU?



Kwa kauli hii unapata picha kuwa Walitumwa na Miungu tofauti.


Kauli ya mwisho ya YESU NI HII


17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu (YOHANA 20:17)




MUNGU NI BABA YAKE, PIA NI BABA YETU. Huo ndio ukweli.

HUO NDIO UKWELI.

Aliyemtuma  YESU ni Tofauti na aliyemtuma Muhammad.


Huo ndio utofauti wao.
Mmoja ana mwana mwingine hana.



KAULI YA WA KWANZA HAIWEZI kupingwa baada ya miaka 600




TAMBUA KUWA ALIYEMTUMA YESU ANAKUBALI KUITWA BABA, Hii ni tofauti na aliyemtuma Muhammad.