Jumanne, 28 Februari 2017

Ufalme wa Mungu umekaribia.

Ni jambo jema kuwaambia watu kuwa ufalme wa Mungu umekaribia, kulingana na maelezo ya YESU.
HABARI za ufalme wa Mungu ni njema, Ila sharti lake huambatana na
Marko 16
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
Usipoamini bado huwezi kuwa na tumaini la kuingia katika ufalme wa MUNGU (MBINGUNI)
Na unapoamini inatakiwa UBATIZWE, ILI KUZIKA DHAMBI NA UTU WA KALE, NA HIVYO KUWA KIUMBE KIPYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.
Marko : Mlango 1
15 akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili.
Ukishaamini na kubatizwa, uksachana na dhambi, endapo ukitenda dhambi inatakiwa Utubu upesi ili uirudie hali ya kukubarika mbele za Mungu muumba MBINGU na dunia na vyote vilivyomo.
YESU ASISITIZA JUU YA KUBATIZWA (KUZALIWA MARA YA PILI)
YOHANA  Mlango 3
1 Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.
2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.
3 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili.
8 Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.
NI wajibu wako kutii maagizi ya YESU KUHUSU INJILI.
Natumai umejifunza kitu, usiwe na roho ngumu naomba utubu, uiamini Injili na kutenda Sawa saw a na MAPENZI YA MUNGU, HAKIKA HUTAJUTA.
Mungu akubariki, pia akujalie kuijua INJILI IOKOAYO SIKU ZOTE,
                                       AMINA.

KAZI ya MTU hupimwa mwishoni siyo mwanzoni

BWANA YESU APEWE SIFA SANA SANA

KAZI YA MTU ALIYOPEWA NA MUNGU UPIMWA MWISHONI SIO MWANZONI NA KUPEWA MALIPO

KUTOKA 39:32-43

Mungu uwa anapima kazi aliyokupa kuifanya kuhanzia mwishoni yaan pale ulipomalizia ndio hapo Yeye uwa anahesabu kuwa umefanikiwa kuifanya ,mwisho wa kumalizia kazi aliyokupa n bora kuliko mwanzo wako

👉Alafu mtu anapo maliza kuifanya Mungu uhanza kutazama je amefanikiwa kuifanya kama moyo wake ulivyotaka ,haijalishi n kazi gan nzuri umeifanya dunia lakin kama aiendani na kusudi lake LA moyon mwake hapo ujue Mungu atakukataa wewe pamoja na ulichokifanya

👉Msisitizo wa Mungu sio kufanya huduma tu Bali je umefanya sawa sawa na mapenzi yake yaan moyo wake unavyotaka au la

👉Bwana Mungu akaniambia "ivi siku ya kubagua watu yaan kutenga kondoo na mbuzi inakaribia sana wengi wataniambia kuwa Bwana je hatukufanya miujiza na kutoa pepo kwa jina lako naye atawaambia ondoken nyie watenda maovu ,sikuwajuha kamwe , niliposikia hayo maneno nilijiuliza moyoni nkasema Baba Naomba unipe siri ya kuwakataa wale waliofanya matendo na huduma kwa jina lako na ukawakataa mwishoni ndipo kama vile alijuha swali langu moyoni mwangu akanijibu ivi akasema "Ni matendo yao ,matendo ndio yatawafanya niwakatae siku ile " Matendo yao yalikuwa kinyume na YESU wao kwaiyo YESU kumbe hatazami tuu ufanyaji wako wa kazi bali  anatazama je unaenenda sawa sawa na mapenzi yake ,je kile unachofanya kimebeba kusudi la Mungu wako

Ukisoma mstari 43-42👉Unaona kuwa walipata heri au baraka mwisho kwa sababu walifanya vile vile kama Mungu alivyo mwagiza Musa na ndipo neno heri au baraka likatoka juu yao
Msisitizo wa Mungu n kufanya kazi au huduma ya Mungu wako sawa sawa na mapenzi yake

Mungu atusaidie tusije kuwa mbuzi badala ya kondoo ,tutakapo ufikia mwisho wetu

Ule mwisho nao unasogea sana sana

BWANA YESU KARIBU ANAKUJA TUKAE MACHO

MAMLAKA YA YESU

Ndugu msomaji karibu katika blog hii ujifunze, Mungu akusaidie use na moyo wa kujifunza Neno lake na uuishi wokovu.