Jumatano, 10 Mei 2017

MOYO WA MTU HUAMBATANA NA MUNGU AU MALI.

MOYO WAKO UMEAMBATANA NA MUNGU AU MALI

HALELUYA

Mathayo 19;16~24

16 Na tazama mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu nitende jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?
17 Kwani kuniuliza habari ya wema? Alieye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima zishike amri
18 Akamwambia zipi? Yesu akasema, Ni hizi usiue,usizini,usiibe,usishuhudie uongo,
19 Waheshimu baba yako na mama yako na mpende jirani yako kama nafsi yako.
20 Yule kijana akamwambia, haya yote nimeyashika nimepungukiwa na nini tena?
21 Yesu akamwambia ukitaka kuwa mkamilifu enenda ukauze ulivyo navyo uwape masikini nawe utakuwa na hazina mbinguni kisha njoo unifuate
22 Yule kijana alipo sikia neno lile akaenda zake kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Yesu akawaambia wanafunzi wake amini nawaambieni ya kwamba itakuwa shida tajili kuingia katika ufalme wa Mbinguni
24 *Nawaambia tena ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu*

Bwana Yesu apewe sifa sana

Tumesoma habari ya yule kijana tajiri anamuuliza Yesu kwamba afanye nn aulithi ufalme wa mbinguni. Kijana alipenda kwenda mbinguni na ndio maana anamuuliza Yesu kwamba afanye nn ili aingie mbinguni Yesu anamuuliza kama anazijua amri kijana alimjibu kuwa yote ameyashika na anayafanya sasa kwa kuwa alikuwa na shauku ya kutaka kuingia mbinguni anamuuliza nimepungukiwa nn tena kama ni amri anazijua na anayafanya ingekuwa ni mtu mwingine ingewezekana kwa kuwa Yesu amemwambia amri na anazijua angeishia hapo kuuliza angesha jua mbingu yangu lkn kijana akawa na shauku ili ajua labda kama amepungukiwa kitu kisimfanye aende mbinguni na Yesu ndipo anamjibu na Yesu aliijua shauku ya kijana na aliona kabisa huyu anapenda kwenda mbinguni na alijua pamoja na kijana kutaka kwenda mbinguni yulr kijana moyo wake ulikuwa haujashikamana na nae ila umeshikamana na mali ndipo anamwambia kauze vyote ulivyo navyo ukawape maskin kisha unifuate. Kijana aliondoka kwa huzuni sababu moyo wake ulikuwa kwenye mali na sio Mungu na ndio maana jibu la Yesu lilimfadhaisha sana. Ni kweli kijana alitaka kwenda mbingun lkn moyo haukuwa na Mungu bali mali
Yesu alipo kuwa anamwambia kijana akauze mali zake hakuwa na maana amfilisi ila alitaka kujua kama kweli moyo wake umeshikamana naye

Mpendwa Mungu anapo tuambia tumtolee sadaka si kwamba amataka pesa zetu sababu vyote ni mali yake anataka kupima mioyo yetu kama kweli tunampenda Mungu na kujitoa hata kwa mali kwa ajili yake. Na ndio maana anasema tutoe kwa hiyari yaan mioyo ya kupenda lkn pia maandiko yanasema hazina na mtu ilipo na moyo wake ulipo inamaana ww ukitoa kasehemu kadogo ka mali zako ndio kaupendo kako kalivyo kwa Mungu

Hebu tusome mf huu kwa baba yetu Ibrahimu tuone jinsi sadaka ilivyo na nguvu na Mungu jinsi anavyo tupima

Mwanzo 22;1~12
Hapa tunasoma habari za Ibrahimu. Mungu alimjaribu akamwambia amtoe sadaka mwanae wa pekee si kwamba Mungu alikuwa akimtaka Isaka na si kwamba Mungu alikuwa hajui kama Ibraimu hamchi yeye ila alimjaribu kuupima moyo wake kama kweli Ibrahimu anampenda Mungu kwa moyo wake na Mungu alithibitisha hilo kwamba kweli.Ibrahimu anampenda kwa maana hakumzuilia mwanae wa pekee alitaka kumchinja soma mstr wa 12

Hivyo mpendwa Mungu akikusemesha kwa habar ya kutoa hata kiwe kitu muhimu vip kwako toa sababu Mungu haitaji hicho anahitaji ule utayari wako wa kujitoa kwa moyo kwa ajili yako.

Je moyo wako.umeshikamana na nani Mungu au mali au kazi kama ni Mungu jipime unavyo jitoa kwa ajili ya Mungu ile kwa mali au muda hicho ndicho kitakacho kuthibitishia unampenda Mungu hebu muangalie mama mjane alitoa senti mbili lkn Yesu alimuona ametoa kuliko wote sababu hakutoa sehemu ya mali bali alitoa kwa moyo tena chote alicho nacho Mungu.anaangalia moyo wako unavyo jitoa angalii kiasi unachotoa na moyo ndio kipimo cha ww unampenda Mungu

kijana alishindwa kuendelea na Yesu sababu alikuwa na mali nyingi sana na moyo wake ulikuwa kwenye mali alizo nazo sio kwa Yesu

Je ww moyo wako uko wapi?
Je unampenda Mungu kweli?
Je unajitoa kiasi gani kwa ajili ya Mungu

Ibrahimu Mungu alipo uona moyo wake kwamba anamcha Mungu akumzuilia mwana wake wa pekee Mungu alimbariki Ibrahimu alitengeneza agano nae mpaka leo watu tujajibarikia katika uzao wake taifa la Israeli

SADAKA YAKO IAMBATANE NA MOYO WAKO NA MOYO WAKO UAMBATANE NA BWANA SI MALI.

Amosi 3;3 je! watu wawili waweza kutembea pamoja wasipokuwa wamepatana?
Hauwezi kutembea na mtu pasipo kupatana naye. Namaanisha Huwezi kutembea na Mungu au kuwa karibu na Mungu wakati moyo wako upo mbali nae na moyo wako kuwa karibu nae ni vile unavyo jitoa kwa ajili yake(MUNGU)  na kutembea katika sheria zake.

ROHO MTAKATIFU aendelee kukufundisha.

Barikiwa .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni