Alhamisi, 9 Machi 2017

JINSI WANAFUNZI WA YESU WALIVYO KUFA

JINSI WANAFUNZI WA YESU WALIVYOKUFA.!

1. #Mathayo.
Huyu aliuawa kwa upanga huko Uhabeshi (Ethiopia ya leo) baada ya kuonyesha imani kali kwa kutetea kanisa. Alijeruhiwa kwa upanga na kidonda chake hakikupona hadi umauti ulipomfika.

2. #Simoni_Zelote (Mkananayo)
Huyu alifariki huko Alexandria Misri ya sasa baada ya kuangushwa na farasi barabarani, aliangushwa vibaya na hakupata msada. Mwishowe akafariki.

3. #Filipo
Alinyongwa huko Ugiriki, hii ni kutokana na msimamo wake mkali aliouonesha dhidi ya Kristo.

4. #Yohana (nduguye Yakobo)
Huyu alitumbukizwa katika pipa lenye mafuta yanayochemka huko Roma, (Italia ya sasa). Hata hivyo kwa miujiza hakuungua na  alitolewa akiwa mzima kabisa.

Alipelekwa katika gereza lililokuwa katika migodi huko kisiwa cha Patmos. Na huko ndiko alipofunuliwa na mwenyezi Mungu na kuandika kitabu cha "Ufunuo wa Yohana". Baadae aliachiwa huru na kwenda kutumika kama Askofu huko Edessa (Uturuki ya sasa). Alifariki akiwa mzee sana. Na ni mtume pekee aliuefariki bila mateso.

5. #Simoni (Petro)
Huyu alipata adhabu ya kifo cha msalaba. Ila yeye alisulubiwa tofauti na Yesu kristo. Kusulubiwa kwa Petro ilikuwa kichwa chini miguu juu katika msalaba wenye nembo ya "X". Petro mwenyewe aliomba asulubiwa kwa namna hii kwani hakutaka kusulubiwa kama Yesu (Yohana 21:18)

6.#Yakobo (wa Alfayo)
Alikuwa Kiongozi wa kanisa huko Jerusalemu Israel ya sasa. Yeye alitupwa kutoka juu kabisa ya mnara wa hekalu wenye urefu wa meta 100 baada ya kugoma kumpinga Kristo. Mnara huo ni ule ambao Shetani aliutumia kumjaribu Yesu kwa kumwambia kama yeye ni mwana wa Mungu ajirushe.  Walipogundua kuwa hajafa baada ya kumdondosha tokea juu ya mnara, walimpiga na mawe mpaka akafa.

7. #Yakobo (mwana wa Zebedayo nduguye Yohana)
Alikuwa ni mvuvi kabla Yesu hajamteua kuwa mwanafunzi wake. Akiwa kiongozi mkubwa wa kanisa lakini alichinjwa huko Yerusalemu kwa kukatwa kichwa kwa amri ya Herode (Matendo 12:2).

8. #Batholomayo
Pia alijulikana kama Nathanieli. Alikuwa ni mmisionari huko Armeni (Asia ya sasa). Alimshuhudia Yesu Kristo huko Uturuki. Yeye aliuawa kwa kupigwa fimbo baada ya kugoma kuacha mafundisho yake dhidi ya Kristo. Alipigwa fimbo nyingi zilizochubua ngozi yake na kutengeneza vidonda. Kisha akawekewa chumvi ktk vidonda hivyo, na kuanikwa juani hadi mauti ilipomfika.

9. #Andrea
Aliuawa kama Petro huko Ugiriki kwa kusulubiwa kwenye msalaba wenye umbo la "X" miguu juu kichwa chini sawa na Petro Petro. Ila baada ya kuwambwa msalabani aliendelea kupaza sauti akihubiri neno la Mungu mpaka mauti ilipomchukua. Akiwa msalabani aliwaambia wafuasi wake "nilikua naisubiri sana saa kama hii"

10. #Tomaso
Aliuwa kwa kupigwa na mshale huko Chennai (India ya sasa) katika moja ya safari zake kama Mmisionari kwenda kuanzisha Kanisa huko.

11. #Yuda (Thadayo)
Aliuawa kwa kupigwa na mshale ubavuni.

12. #Yuda (Iskariote)
Huyu alijiua kwa kujinyonga baada ya kumuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha. Alinunua shamba kwa zile fedha alizomuuza nazo Yesu. Lakini alijinyongea kwenye shamba hilohilo. Kamba aliyojinyongea ilikatika na akaanguka na tumbo lake kupasuka na matumbo kutoka nje. Shamba lile likaitwa "Akel Dama" yani Shamba la damu (Matendo 1:18-19).

NOTE:
13. #Mathia
Ni Mwanafunzi aliyechaguliwa kuziba nafasi ya Yuda Iskariote (msaliti). Alipigiwa kura na wanafunzi 11 wa Yesu baada ya kifo cha Yuda (Matendo 1:26). Huyu alipigwa na mawe  hadi kufa na baada ya hapo walimkata kichwa.

14. #Paulo
Hakuwa mmoja wa wale wanafunzi 12 wa Yesu. Lakini huhesabika kuwa mfuasi wa Kristo na mtetezi wa mwanzo wa Kanisa. Huyu aliteswa na baadaye akachinjwa na Emperor Nero huko Roma mwaka 65 (A.D).

Kabla ya kuchinjwa Paulo aliishi muda mrefu sana gerezani ambapo akiwa huko aliandika barua (nyaraka) nyingi kwa makanisa mbalimbali. Ndio hizi ambazo zinafundisha misingi ya ukristo katika agano jipya, kama vile Waraka wa Paulo mtume kwa Warumi, Wakoritho, Waefeso, Wakolosai, Wathesalonike, Timotheo etc.

NB: Si muhimu kujua ni namna gani mitume walikufa, ila ni muhimu kujua kuwa mitume wote walikufa wakitetea imani yao. Walikua tayari kuchukiwa na kufa vifo vya mateso kwa ajili ya kumtetea na kumshuhudia Kristo.

Biblia imesema, "Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu, lakini mwenye kuvumilia mpaka mwisho, ndiye atakayeokoka." Mathayo Mtakatifu 10:23

MUNGU AKUBARIKI

USIWE KWAZO KWA NAMNA YOYOTE ILE

USIWE KWAZO LA NAMNA YEYOTE

Bwana YESU atukuzwe mpendwa wangu.

Karibu tujifunze Neno la MUNGU.

Wakati mwingine si mara zote watu hukulaumu kwa kukusingizia, wakati mwingine jichunguze ili usiwe laumu au kwazo pasipo sababu.

2 Kor 6:3-10 '' Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe;  bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa MUNGU; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida; katika mapigo, katika vifungo, katika fitina, katika taabu, katika kukesha, katika kufunga; katika kuwa safi, katika elimu, katika uvumilivu, katika utu wema, katika ROHO MTAKATIFU, katika upendo usio unafiki; katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto; kwa utukufu na aibu; kwa kunenwa vibaya na kunenwa vema; kama wadanganyao, bali tu watu wa kweli; kama wasiojulikana, bali wajulikanao sana; kama wanaokufa, kumbe tu hai; kama wanaorudiwa, bali wasiouawa;
kama wenye huzuni, bali siku zote tu wenye furaha; kama maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote.''

Mtumishi wa MUNGU hapaswi kuwa kwazo.

Kama watu wanakwazika na wewe basi wakwazike kwa sababu ya injili, na kama wanakwazika kwa sababu ya injili basi wewe sio kwazo maana hujawakwaza lolote ila Neno la MUNGU ulisemalo ndilo limewakwaza, na Neno la MUNGU limekamilika na limejitosheleza ili kumsaidia mwanadamu haijalishi anakwazika au anafurahi.

Mtumishi wa MUNGU hutakiwi kuwa mtu wa kusambaza maneno ya uongo maana kwa hayo utakwaza watu.

Mtumishi wa MUNGU hupaswi kuwa mnafiki maana kwa unafiki huo utakwaza watu.
Kama wanadamu wanakusingizia wewe songa mbele maana wao wamekwishapata thawabu yao duniani na wewe endelea kuichuchumilia thawabu ya mbinguni yenye uzima wa milele katika Wokovu wa KRISTO..
YESU KRISTO akusaidie kama unaendelea kumtumainia yeye Mfalme wa Uzima wa milele ila usikubali kuwa kwazo.

Luka 17:1-4 '' Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!  Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa. Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe. Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.''

Kuna baadhi ya watu wa kanisa wamegeuka kwazo hata kwa imani maana wanaipotosha kweli.

Unakuta mtumishi anaombea kwa pesa, huko ni kuwa kwazo na ni uovu.

Mathayo 10:8 '' Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.''

Badala ya kuulinda ufalme wa MUNGU wewe unauuza ufalme wa MUNGU?
Umekuwa Mkristo mbaya, umejitenga na KRISTO kwa kufuata tamaa zidanganyazo.
Umekuwa mtumishi mbaya, umejitenga mbali na KRISTO kwa kufuata tamaa zidanganyazo.

Wengine pia wamekuwa makwazo yanayosababisha hata watu waende jehanamu kwa sababu yao.

Wengine hata kweli inatukanwa kwa ajili yao kwa sababu ya uovu wao.

Kila Mteule wa KRISTO ni mtumishi wa MUNGU hivyo haiwapasi watumishi wa MUNGU kuwa makwazo ya kweli ya kuwafanya watu wasije kwa YESU hata wapate uzima.
Ni Mara ngapi umeikataa dhambi kama Yusufu alivyoikataa dhambi?
Ni Mara ngapi umeikimbia dhambi iliyokuwa inakunyemelea?
Ndugu yangu ni muhimu sana kuikataa dhambi na kuikimbia dhambi.
Kumbuka dhambi ni uasi kwa MUNGU, hivyo hatutakiwi kuwa waasi kwa MUNGU.

" Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza KRISTO; ikiwa mlimsikia mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika YESU, mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu;
mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya MUNGU katika haki na utakatifu wa kweli. Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake. Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi. Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji. Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia. Wala msimhuzunishe yule ROHO MTAKATIFU wa MUNGU; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya; tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na MUNGU katika KRISTO alivyowasamehe ninyi.-Waefeso 4:20-32"

Mtu mwingine anaweza kugeuka kwazo kwa sababu hajifunzi Neno la MUNGU hata akue kiroho.

Unakuta mtu ameokoka na huu ni mwaka wa 15 lakini hata akiambiwa kufunga masaa 12 tu hawezi.

Ndugu zangu ni muhimu kujua kwamba Mtu anayekua kiroho ni mtu yule anayejituma mwenyewe katika yaliyo ya KRISTO na MUNGU.

Warumi 12:11 "kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia BWANA;"

Je wewe unakua kiroho au umedumaa?
Je unakua kiroho au unashuka viwango vya kiroho?

Ukitaka kukua kiroho chukua kanuni ambayo ya Warumi 12:11  na zingatia maelekezo ya andiko hilo itakusaidia.

Kuna watu pia wamegeuka makwazo kwa sababu tu ya kutetea uovu.

Unakuta Mchungaji anatetea pombe.

Unakuta mtumishi anasifia nyimbo za kidunia.

Unakuta Mtumishi kwa sababu tu ya mapenzi yake kwa chama fulani au taasisi fulani ya kidunia au dhehebu fulani basi hutetea hata ujinga unaofanywa na kikundi hicho au kanisa hilo kwa sababu tu ni watu anaopendezwa nao.

Ndugu pendezwa na Neno la MUNGU na sio machukizo.

Je unaitetea kweli ya MUNGU au unatetea machukizo?
Ndugu, katika utumishi wako hakikisha unaitetea kweli ya injili ya KRISTO.

Hakikisha unakuwa muombaji na  kesha macho ya rohoni.
Omba MUNGU akupe macho ya rohoni ya kukesha.
Hata wakati umelala kimwili lakini macho ya rohoni ya kukesha huona kinachoendelea kwenye ulimwengu wa roho wakati huo.

1 Thesalonike 5:17 '' ombeni bila kukoma;''

Je unataka kufanikiwa katika maisha yako?
Je unataka kufanikiwa kiroho na kimwili?
Jambo muhimu mpokee YESU kama hujampokea.
Ishi maisha matakatifu katika yeye na zingatia hii huku ukihakikisha kwamba wewe sio kwazo la kutafuta pesa kitapeli;

Mithali 16:1-3 "Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA. Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe; Bali BWANA huzipima roho za watu. Mkabidhi BWANA kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika."

Najua una matarajio mengi sana lakini kama huna YESU moyoni mwako ni hasara kwako. Biblia inasema

"Usijisifu kwa ajili ya kesho; Kwa maana hujui yatakayozaliwa na siku moja. Mwingine na akusifu wala si kinywa chako mwenyewe; Mtu mgeni wala si midomo yako wewe.-Mithali 27:1-2

Ukiwaza ushindi waza pia na utakatifu na hakikisha ushindi wako unambatana na utakatifu.
Ukiwaza ushindi katika MUNGU hakikisha unadumu katika utakatifu ndani ya Wokovu wa YESU KRISTO utafanikiwa.
Lakini katika yote usikubali kuwa kwazo kwa kanisa au jamii.

Vyanzo vya mtu kuwa kwazo ni.

1. Roho ya kiburi.

  1 Petro 5:5 inasema ''...MUNGU huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.''

Kiburi ndio maana wa dhambi zote.

Kwa kiburi kunaweza kutokea makwazo mengi sana.

2. Dhambi.

1 Yohana 3:4 '' Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.''

Dhambi hutengeneza mambo mengi na hata kuna makwazo huja baada ya dhambi.

Fikria mwanakwaya anafanya uzinzi na kwaya nzima inaonekana ni wazinzi, na hata nyimbo zao wakiimba kanisani watu huona kama wanapoteza tu muda maana wanajulikana ni wazinzi wakati mzinzi ni mmoja tu na huyo amegeuka kwazo kwa kikundi kizima.

3. Kujihesabia haki.

Mathayo 7:1 ''Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.''

Anayejihesabia haki siku zote huwaona wengine ni wabaya hata kama yeye ndiye mbaya.

Anaweza akawahukumu wengine hata kama yeye ndiye anapaswa kuhukumiwa.

4. Kujiona bora kuliko wengine.

Wafilipi 2:3 ''Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.''

Ukijiona wewe ni bora kuliko wengine unakuwa unapishana Neno la MUNGU linalokutaka uwahesabu wengine ni bora kuliko wewe.

Ukijiona bora kuliko wengine hakika hutakuwa na unyenyekevu na kwa njia hiyo utageuka tu kwazo katika sehemu sehemu.

Kuna watu hata hawawezi kuwatii wachungaji wao kwenye kweli ya MUNGU na kwa njia hiyo hugeuka makwazo.

Kuna watu hata huwafuata baadhi ya washirika ili kuwarubuni ili wasifanye jambo fulani jema la kikanisa lililopagwa, kwa sababu tu wao hawakupewa kusimamia, huko ni kujiinua na kujiona bora na kwa njia hiyo mtu kama huyo lazima awe makwazo tu.

5. Tamaa.

Yakobo 1:14-16 ''Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti. Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike.''

Ndugu tamaa zako mbaya zinaweza kuleta makwazo kwa jamii au kanisa au familia au majirani.

Usikubali kuwa kwazo lolote kwa sababu tu ya tamaa zako za kipepo.

Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.

MUNGU AKUBARIKI

Jumatano, 8 Machi 2017

U HERI, ISRAEL

kumbukumbu la torati : Mlango 33

29 U heri, Israeli.Ni nani aliye kama wewe, taifa lililookolewa na BWANA!Ndiye ngao ya msaada wako,Na upanga wa utukufu wako;Na adui zako watajitiisha chini yako,Nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.

Jumanne, 7 Machi 2017

MWALIKO WA SADAKA TOKA KWA MUNGU

Mwakasege.

Mwaliko wa sadaka toka kwa Mungu

Utoaji wa sadaka ni mwaliko binafsi utokao kwa Mungu ili ukutane nae. 2Wakorintho 9:6-7 “Lakini nasema  neno  hili apandae haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna ukarimu. Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni wala si kwa lazima, maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu,”

 Kwa maana kutoa ni moyo, Mungu  akikutana na moyo wako anaangalia na Imani uliyo nayo. Hajalishi umekuja na sadaka kiasi gani. Mtu mwenye Imani ana uhakika ya kwamba ameona na hivyo basi utoaji wako wa sadaka usiegemee ni kwa jinsi gani umeskia mahubiri bali yale maelekezo uyasikiayo toka kwa Mungu ndani ya moyo wako.

Kum 12:10-14 “Lakini mtakapovuka Yordani na kukaa katika nchi anayowarithisha BWANA, Mungu wenu, akawapeni raha, akiwaokoa na adui zenu pande zote mkakaa salama; (11) wakati huo itakuwa kwamba mahali pale atakapopachagua BWANA, Mungu wenu, alikalishe jina lake, hapo ndipo mtakapoleta kila kitu ninachowaamuru; sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu zote teule mtakazoweka kwa BWANA. (12) Nanyi mtafurahi mbele za BWANA, Mungu wenu, ninyi na wana wenu, na binti zenu, na watumishi wenu wanaume na wanawake, na Mlawi aliyemo mlangoni mwenu; kwa kuwa hana sehemu wala urithi kwenu. (13) Ujihadhari usitoe sadaka zako za kuteketezwa katika kila mahali upaonapo; (14) bali katika mahali atakapopachagua BWANA katika kabila zako mojawapo, ndipo utakapotoa sadaka zako za kuteketezwa, ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo,”

Kama maandiko yanavyosema hapo juu utoaji wa sadaka ni Mwaliko toka kwa Mungu. Katika utoaji wa sadaka unafuata maelekezo ya Mungu na hii ina maana unatoa kwa Imani. Hutoi sadaka kama unavyotaka wewe bali maelekezo ya Mungu  ndiyo yakuongozayo. Huwezi toa sadaka kwa sababu watu wana shida, lakini msaada unawza toa. Kama mstari wa 13 unakupa onyo kabisa kwamba ujihadhari usitoe sadaka zako za kuteketezwa kila mahali upaonapo. Na mstari wa 14 unaonyesha utoe sadaka mahali ambapo Mungu amekuelekeza.

Ntajuaje kuwa hapa ndo bwana alipochagua?

Pale BWANA alipoamua kulikalisha jina lake ndipo unapotakiwa kutoa sadaka zako. Kama kitabu cha Mathayo 18:20 kinavyosema  “Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, name nipo papo hapo katikati yao”. Kama mahali ambapo jina lake halipo basi usitoe sadaka. Kwa maana baadhi ya watu wanapenda kutoa sadaka sehemu ambazo wanaona wanapaswa kutoa. Toa sadaka mahali ambapo uwepo wake umekaa. Mathayo 6:21 “ Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako,”. Unapoenda kutoa sadaka sio kwamba Mungu ana shida nayo bali anataka kukutana na moyo wako. Kama ni Kanisani Mungu atakuonyesha kanisa gani. Na ikumbukwe kwamba Imani huja kwa kuskia na sio kila asikiae ana imani. Muombe Bwana auhidhirishe uwepo wake kwako.

Ni makosa kwa kanisa kufikiri linaweza kutengezea heshima ya Mungu katika jamnii. Ni Mungu pekee ndo anaweza kufanya hivyo. Elia alipoomba akasema na ijulikane leo ya kwamba mimi ni mtumishi wako na nimefanya kila kitu sawa sawa na neno lako.

Maneno haya maana yake kuna nguvu za Mungu zinakuweko mahali halafu zinanyamaza, unatakiwa uziactivate.  Kule kunyamaza sio kwamba hazipo.  Na kuactivate/kuziamsha kwake ni kwa kutoa sadaka kwa kusema na ijulikane leo kwa maana utakutana nae (MUNGU). Sema na Mungu ya kwamba unataka Ijulikane leo unapotoa sadaka.

Mungu nataka ijulikane leo unapotoa sadaka hii. Ukisoma  biblia KUTOKA 25:1-23  kuhusiana na ujenzi wa hema jiulize Mungu alipokuwa anaagiza hii sadaka alikuwa anataka nini? Sio kwamba Mungu alikuwa na shida nayo bali hitaji lake ni kutafuta mahali pa kukaa kama mstari wa nane unavyoonyesha wazi “Nao wanifanyie patakatifu, ili nipate kukaa kati yao”.Kwa maana hiyo hitaji la Mungu katika kutoa sadaka si sadaka bali anatafuta mahali pa kukaa.

 Kwa sababu alikuwa haihitaji (angalia mstari wa 8). Tafuta sababu ya Mungu ya kukuambia utoe sadaka. Hitaji la Mungu katika kutoa sadaka si sadaka bali anatafuta a DWEILLING PLACE yaani mahali pa kukaa! KUTOKA 29:42,43 “itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa milele katika vizazi vyenu vyote mlangoni pa ile hema ya kukutania mbele ya BWANA; hapo nitakapokutana nanyi, ili ninene na wewe hapo. Nami nitakutana na wana wa Isreaeli hapo, na hiyo hema itafanywa takatifu na utukufu wangu”

Utakatifu/Utakaso is to be set apart for the purpose of God. Utukufu wa Mungu ni uwepo wa Mungu uliofunuliwa. Kama unaamini Mungu anaponya lazima kuwe na manifestation kwenye physical being. Hema ni presence ya Mungu. What sets a person apart is the presence of God. Kwa mfano, Kama mhubiri hana anointing juu yake, akihubiri sehemu yenye anointing huhubiri tofauti na watu kusema Yule mhubiri  mbona kwake hajawahi kuhubiri kama hivi? Ikumbukwe kwamba sio yeye bali ni uwepo wa Mungu umemuwezesha kutoa mafundisho ya kipekee tofauti na akiwa kanisani kwake, sio yeye ni Presence ya God imemuwezesha kutoa mafundisho kama hayo.

Mbarikiwe!

HALI YA KIROHO YA ARHI INAYOHUSIKA NA KUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO sehemu 2

2⃣SOMO: *HALI YA KIROHO YA ARDHI INAVYOHUSIKA NA KUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO*

ENEO: *DAR ES SALAAM*

SIKU: 2 March, 06 2017

MWL. C. MWAKASEGE

*TANGAZO MUHIMU*
👌🏽Jumamosi asubuhi kama una huduma ya ualimu hata kama hujui njoo kuna mafundisho na shule ya ualimu kujua na kutambua

👌🏽Na tarehe 14 May Diamond Jubilee siku ya vijana

👌🏽Kila siku maombi yatakuwa yanafanyika mahali hapa kufuatana na somo la siku hiyo

👌Semina pia iko live katika
Channel ya *Swahili Africa* ambayo inapatikana ktk king'amuzi cha Azam channel 120 startimes channel 121.

Itakuwa LIVE ktk siku zote ambazo semina itakuwa inaendelea hapa viwanja vya Tanganyika parkers Kawe Jijini Dar es salaam

https://youtu.be/ryFv_R47ScM
👆👆Semina ya Jana(Video)

*LENGO YA SOMO:*
Kuhakikisha ya kwamba Mafanikio yako yaliofungwa kwenye hali ya kiroho ya ardhi yanafunguliwa

*Kumb 6:12, 2Nyk 7:14*

✅Pitia somo la jana ili kujua tulipotoka na yale mambo ya msingi 5 juu ya kufungua mafanikio yako yaliyofungwa na hali ya kiroho ya ardhi inayofanya mahali unapoishi pawe nyumba ya utumwa

Day 1: https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=1288841767871251&id=100002363196786

👆👆Summary

✅Kumbuka jambo la msingi utumwa wa wana wa Israel  haukuwa kwa sababu ya kazi walizokuwa wanafanya bali ni kwa ajili ya hali ya kiroho ya mazingira ya kazi walizokuwa wanafanya

✅Walimlilia MUNGU juu ya uchungu mioyoni mwao wakati wanafanya kazi wala si kwa sababu ya kazi kuwa ngumu

➡Leo tuangalie *NAMNA YA KUJIONDOA KWENYE MADHARA YA LANGO YA ARDHI YA NYUMBA UNAYOISHI INAPOMILIKIWA KIROHO YA NGUVU ZA SHETANI*

➡Ni jambo pana na jipya kwa watu wengi neema ya MUNGU na iwe juu yako kuweza kuona na kufahamu jambo hili maana kujua na kufunguliwa katika jambo hili utafunguliwa katika mambo mengi sana

*Esta 8:1-2, 13-14*
*Mwz 22:17*
*Math 12:29*
*Kut 12:12-23*

*Tuangalie vipengele vichache vya jambo hili ili iwe rahisi kuelewa*

1⃣Ardhi na nyumba iliyojengwa juu yake vina uhusiano wa kiroho

➡Unasema unajuaje…..?

➡Kufuatana na *Kumb 6:12* MUNGU amelinganisha nchi na nyumba kwa hiyo ardhi ile ambayo ina mipaka halali inauhusiano wa kiroho na nyumba inayojengwa

2⃣Mlango wa nyumba una uhusiano na mlango wa ardhi

➡Kwanini? sababu kama ardhi ina uhusiano wa kiroho na nyumba basi na milango yao ina mahusiano

3⃣Ukigusa mlango wa ardhi kiroho unagusa pia mlango wa nyumba kiroho

*Matendo 16:26*

➡Tetemeko lile halikuwa la kawaida lile la kuangusha nyumba bali lilikuwa lile la kushughulika na ardhi ambayo juu yake gereza lilikuwa lipo

➡Sababu walikuwa wapo gerezani kwa jinsi ya mwili isingekuwa rahisi wao kutoka maana hawakufungwa kimwili bali kesi yao mpaka kufungwa kwao ilikuwa kiroho

➡Ndiyo maana MUNGU alileta tetemeko akatikisa misingi ya gereza na Biblia inasema milango ya gereza ikafunguka haisemi ikavunjwa na vifungo walivyokuwa wamefungwa vikaachia

➡Yule askari alipoona milango iko wazi alitaka kujiua maana alijua wametoroka lakini walimwambia asijiue akawakaribisha kwake akawanawisha miguu na kuwatayarishia chakula na baada ya hapo walirudi gerezani

➡Kulipokucha asubuhi wale makadhi waliowafunga walitoa order ya wakina Paulo kuachiliwa.

➡Nini nataka uone hapa gereza halikuvunjwa wala kuwa na nyufa hata moja kutoka kwenye lile tetemeko
MUNGU hakuwa na shida na gereza la nje bali alikuwa na shida na gereza la kiroho ambalo kwa jinsi ya nje watu wanaona kama vile kuta tu na linaweza kuwa sehemu yoyote ile

➡MUNGU alikuwa anashughulika na ardhi  ili kushughulika na nyumba iliyo juu ya ardhi akafungua milango ya ardhi ili kufungua milango ya gereza iliyoko juu yake

➡Kama nyumba yako ni ya utumwa imezungukwa na mazingira ya utumwa usihangaike kuombea nyumba bila kuombea ardhi ya nyumba hiyo maana mlango wa ardhi una uhusiano na mlango wa nyumba yako

➡Vita ya ardhi si vita ya kumshirikisha kila mtu maana ina mapamabano yake mabaya kama hujajipanga

➡Kama huna NENO la kutosha ndani yako MUNGU akikusemesha huwezi kusikia maana kusikia huja kwa *NENO la KRISTO* maana waweza kushughulika na ardhi MUNGU akikwambia shughulikia mlango la ardhi

➡Wakina paulo walienda kuhubiri wakatengeneza mahali pa kusali bila kucheck na kushughulikia nani anamiliki lango la ardhi/nani ni mmiliki wa lile eneo

➡Waulize watu wa nyumba ya Hamani maana kiroho nyumba yake ilikabidhiwa Esta na Modekai sasa haijalishi kikao cha mirathi kimeamua nini maana wamiliki ndio wanaoamua na kutoa ruhusa hali ya kiroho na hali ya maisha ya nyumba hiyo inaendaje

➡Unaanzisha kanisa/fellowship mahali badala ya kuangalia na kucheck nani ameshikilia lango la roho nyingine inayopingana na kitu unachofanya na ambaye ameshikilia lango la ardhi ambalo pia ndilo limeshikilia lango la nyumba ya sehemu hiyo na msingi wa kiroho unayotumia kusali sasa kama vifungo hivi vimefungwa kwenye ardhi na vikaja kuonenakana mpaka kwa nje usipojua namna ya kuvifungua kwenye ardhi uwezi kufunguka

➡Angalia habari ya kina Paulo  kama waliendele na maombi kikundi cha cha ibada kikavurugika wakafungwa jela hata baada ya kutolewa gerezani walifukuzwa kutoka nje ya mji sababu walianzisha huduma mjini bila kusimamia malango ya ardhi ya mji

*Matendo 16:39-40*

➡Walipotoka gerezani walienda kwa Lidya na kukutana na ndugu/wapendwa tu na wale wapendwa waliwafariji tu hawakuwa wa msaada nao wakaenda zao

➡Ndiyo maana chunga sana watu wanaokushabikia huduma wakati hawajui vita unayopitia, chunga sana watu wanakusumizia  front line wakati hawajui kupigana sababu ukifungwa gerezani watakufariji na kukupa pole na kusema tunakuombea na wakati hawajui hata wanachoomba

➡Mji ule ulikuwa na wapendwa lakini hawakuweza kuwasaidia kina Paulo sababu inategemea ni nani aliyeshikilia lango la ardhi kiroho la mji ule.

➡Maana walioshikilia kama hawaitaki huduma kuwa na uhakika itafungwa na watu kuhamia kwenye huduma ama kanisa jingine hata kama wapendwa wapo na usije fikiri watakusaidia watakufariji tu

➡Vikundi vingi sana vya maombi watu hawajui ni kwanini ghafla vimechanua na ghafla vimekufa sababu ni moja tu ulianzisha kikundi cha maombi bila kushughulikia lango la ardhi ambalo Modekai ndiye aliyeshikilia lango hilo na kama uko kinyume naye kuwa na uhakika kikundi hicho kitafungwa kabisa

➡Ndiyo maana unaweza kukuta makanisa mengine yanapata shida eneo hilo lakini nyumba nyingine hazipati hiyo shida ama kanisa moja linapata shida na jingine wala sasa ni mambo mawili au moja lina operate kwa viwango vya juu sana au siyo tishio

➡Ndiyo maana watu wengi wanapata shida kwenye nyumba zao Biblia inaita nyumba za kitumwa na wako kwao.

➡Umewahi kufikiri kwa mfano hicho kiwanja ulichonunua ni nani anamiliki lango la hicho kiwanja katika ulimwengu wa roho?

➡Nani amepewa kumiliki ardhi uliyojenga? Wengine alipewa marehemu sasa ukichanganya jambo hili kiroho kuwa na uhakika kama usipojua namna ya kutengeneza kisiwa cha ardhi ya kwako utapata shida sana kuvuka na vita yake si nyepesi

4⃣Kama vile nyumba ilivyo na mlango zaidi ya mmoja vile vile na ardhi ina milango zaidi ya mmoja inayoweza kutumika kumfunga mtu

*Isay 26:1-2*

➡Nchi ili kurikaribisha taifa, taifa lazima lipite kwenye lango.

➡Anapozungumzia lango kwenye nchi anazungumzia lango la kwenye ardhi linaloruhusu watu kupitia, kuingia na kutoka

*Matendo 16:26-27, 24*

➡….milango… Biblia haituambii milango ilikuwa mingapi mlinzi alipoamka alikuta milango yote imefunguliwa na funguo anazo yeye.

5⃣Kila lango la kiroho katika ardhi au nyumba lina walinzi wa kiroho

*Matendo 12:6,10*

➡Kulikuwa na walinzi kwa ajili ya Petro  na kulikuwa na walinzi kwa ajili ya mlango/nyumba

➡Kuna mapepo unapewa wewe ukitoka nyumbani unakuwa nayo na kuna yale yamepewa kulinda ardhi ya nyumba yako hayatoki.

➡Alipofika kwa wapendwa waliokuwa wanaomba aligonga mlango (maana yake wakikupa kibali na kukufungulia ingia) malaika halazimishi wapendwa kufungua, wakati huku pengine malaika alimpitisha na milango kufunguka yenyewe. Swala ni kwanini hawakumfungulia? maana yuke dada hakufungua mlango baadaye walikuja wakamfungulia

➡Ardhi ile ilikuwa na malango 4, walipita lindo la kwanza na la pili hata mlango wa chuma na wa kuingilia mjini na mpaka kwa wale wapendwa waliokuwa wanamwombea kuna watu ambao wamefunguliwa lakini wako gerezani.

➡Fikiri Petro kama malaika alipomtokea angemwambia avae nguo na viatu kisha akapotea maana yake nini yuko huru keshavaa nguo na viatu lakini yuko gerezani kafungwa hana uhuru tena

➡Ndiyo maana tuna watu wengi sana tunawaombea na inapofika kwenye kufunguliwa kwao tunafunga mlango tunatamani kuwaona kwenye chumba cha maombi lakini kuwafungulia hatufanyi hivyo.

➡Wengi tunawaombea halafu tukikutana nao tunakumbuka na kuona lile tatizo bado kwako hata kama wamebadilika kwa hiyo tunajikuta bado hatujawafungulia ghafla wanarudi gerezani

6⃣Omba kwa imani na kwa juhudi hadi aliyefungwa apite milango yote iliyomkwamisha

*Matendo 12:5*
*Waamuzi 5:8*

➡Kati ya eneo la uwanja la mapambano la MUNGU ni langoni

➡Petro ililazimika avuke geti 4, mbili ndani ya gereza, moja ndani ya mji na nyingine kwa waliokuwa wanamwombea hivyo MUNGU akikupa eneo la kuwavusha watu na kukupa namna ya kuomba omba mpaka uwavushe geti zote

➡Wakati mwingine unapohitaji msaada wa vita unahitaji watu ambao wanajua kupigana uhitaji msaada wa pole hata kama ni pole bali hawata nyamaza mpaka umetoka

➡MUNGU atakupa mamlaka ya kukanyaga na kupita malangoni na kuachilia *DAMU YA YESU* hapo maana hii ni ahadi ya MUNGU kwa Ibrahimu

*MAOMBI*

Angalia  link hii kule  mwishoni kushiriki maombi

https://youtu.be/ryFv_R47ScM

#MUNGU_akubariki_Mtumishi_wa_MUNGU_Mwl_C_Mwakasege

#Usiache_kumwombea_rafiki

#Usiache_kuombea_semina

#UFALME_KWANZA

*……”Jesus Up”…

Jumatatu, 6 Machi 2017

LAANA NI NINI? NA NINI MADHARA YAKE


IJUE LAANA KWA KINA.

Bwana YESU atukuzwe ndugu.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Laana ni nini?

Laana ni ukosefu wa radhi za MUNGU katika jambo fulani.
Radhi ni nini?
Radhi ni msamaha.
Hivyo laana ni ukosefu wa msamaha wa MUNGU katika jambo fulani.
Hiyo ni maana ya kwanza ya laana.

Maana ya pili ya laana.
Laana ni nini?
Laana ni apizo alitoalo mtu kwa mtu mwingine ili afikwe na mabaya?

Wakristo wengi hujitanganya kwamba hawana laana kwa sababu wamewakombolewa kutoka kwenye laana ya torati.
Wagalatia 3:13-14 '' KRISTO  alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;
ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika YESU KRISTO, tupate kupokea ahadi ya ROHO  kwa njia ya imani.''
Hiyo haina maana kwamba tufanye maovu yanayoleta laana tukijifariji kwamba tumekombelewa kutoka laana ya torati.
Aliyekuambia kwamba torati kazi yake ni kulaani ni nani?
Biblia hapo imeweka wazi kwamba tumekombolewa na laana ya torati ILI BARAKA YA IBRAHIMU AMBAYO MWANZO ILIKUWA NI YA WAISRAELI PEKEYAO, SASA KWA NJIA YA KRISTO YESU BARAKA HIYO INAHUSU WATU WOTE WALIOKOMBOLEWA KWA DAMU YA YESU KRISTO.
Jambo la kujua ni kwamba tumekombolewa kutoka laana ya kutengwa na MUNGU na sasa kwa njia ya KRISTO tunatambuliwa na MUNGU kama warithi sawasawa na ahadi aliyopewa Ibrahimu kwa wanaye.
Wagalatia 3:26-29 '' Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa MUNGU  kwa njia ya imani katika KRISTO YESU . Maana ninyi nyote mliobatizwa katika KRISTO  mmemvaa KRISTO. Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika KRISTO. Na kama ninyi ni wa KRISTO, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.''

Kumbe kabla ya Bwana YESU kutuokoa hatukuwa uzao wa Ibrahimu na hiyo ilikuwa ni laana lakini wana YESU ametufanya sisi kuwa uzao wa Ibrahimu warithi sawasawa na ahadi aliyoapiwa Ibrahimu na MUNGU.
Laana ilipofutika tulihesabiwa haki kama Ibrahimu alivyohesabiwa haki kwa kumwamini MUNGU.
Leo andiko la Wagalatia 3:13 wakristo wengi hulitumia kuonyesha kwamba hawana laana lakini wakati mwingine maisha yao yana laana.
Kuna laana ambazo hutolewa na wanadamu kama maapizo, ndio maana ya pili ya laana na laana hizo zimewakamata wengi kwa sababu hawaombi na hawajui haki zao kwa MUNGU, Wameteswa sana na laana hizo huku wakijifariji kwamba wamekombolewa kutoka laana.
Ndugu zangu ni muhimu kujua kwamba YESU anaweza kukutenga na laana lakini hadi ukiamua wewe kumwita, usipomwita utabaki na laana yako.
Kuna mambo umeyaona kwenye ndoto au maono yakionyesha wachawi au wakuu wa giza wanakulaani, Usipoomba hakika laana hiyo itakupata huku wewe ukibaki kujifariji kwamba umekombolewa kutoka laana.
YESU alisemea ''Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa-Luka 18:1''
Kama huombi hakika laana inaweza kukupata na kukutesa huku ukiendelea kujifariji.
Ndugu mmoja alilaaniwa kwamba  hataolewa, ilipita miaka mingi hadi alipojua kuombea kufuta laana hiyo ndipo aliolewa.
Watumishi wengi kwa sababu labda hawajawahi kupitia laana ndio maana hufundisha kwamba hakuna laana.
Wengine husema kwamba agano jipya halijazungumzia laana lakini wanasahau kwamba Bwana YESU alisema kwamba wenye laana ya MUNGU wataenda jehanamu.
Mathayo 25:41 '' Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;''

=Laana kutoka kwa MUNGU inatengenezwa na dhambi usizotubia hadi kifo chako.
Kumb 28:20 '' BWANA  atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.''
= Laana ya MUNGU pia unaweza ukaipata kwa sababu ya kutokutoa fungu la kumi.
Malaki 3:9 '' Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.''
Kutokutoa zaka kamili ni kumwibia MUNGU na jambo hilo hutengeneza laana.
Wengi hawatoi fungu la kumi wakisingizia kwamba wamekombolewa kutoka laana ya torati wakati Fungu la kumi lipo kabla ya torati. Akina Ibarahimu walitoa Fungu la kumi kwa akina Melkizedeki kipindi ambacho hata torati hajapewa Musa.
Akina Yakobo walitoa Fungu la kumi kabla hata Waisraeli hawajaenda utumwani Misri.
Nikisoma andiko la Mathayo 25:41 kwamba waliolaaniwa na MUNGU watakwenda jehanamu huwa naogopa sana.
Njia ya mbinguni ni nyembamba ndio maana hata kwa zaka tu watu hupishana na njia hiyo ya uzima.

Laana za wanadamu au majini au wakuu wa giza haziwezi kumfanya mtu asiende uzima wa milele lakini laana kutoka kwa MUNGU inaweza kumfanya mtu asiende uzima wa milele.
Laana kutoka kwa wanadamu na mawakala wa shetani zinaweza kusababisha ukateseka katika maisha ya duniani, hivyo ukihisi kuna laana inakufuatilia iwe ni kutoka kwa babu au bibi au mama au baba au mjomba au shangazi au kaka au dada au mtoto wako hakikisha tu unatubu kwa sababu ya kisababishi cha laana hiyo kisha ifute laana hiyo kwa maombi katika jina la YESU KRISTO.
Laana ni jambo baya sana.
Hata makosa ya akina adamu hayakumfanya MUNGU awalaani bali aliilaani ardhi na sio wao.
Je ni lini uliiombea ardhi yao iliyolaaniwa ili laana iondoke kwa damu ya YESU na ufaidike na mazao yanayotokana na ardhi yako?
Bwana YESU analifundisha kanisa lake kupitia Mtume Paulo akisema tusiwe watu wa kulaani watu wengine, ni heri tuwabariki na sio kuwalaani, kuna madhara makubwa yanayotokana na laana hivyo ni heri kubariki tu.
Warumi 12:14-17 '' Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani. Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao. Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.''

Laana ni kitu kinachokukamata ili usifanikiwe kwenye jambo fulani maishani mwako.
Hakikisha laana inaondoka maishani mwako.
Kama ni laana kutoka kwa MUNGU tubu na acha uovu huo kwa kuanza kutenda mema ayatakayo MUNGU.
Zingatia hiyo itakusaidia.
Biblia inasema mtu akilaani mjini basi hata mashambani yaani kijijini atakuwa amelaani.
Kama unasumbuliwa na laana unaweza ukajaribu kufanya biashara mjini lakini hufanikiwi. Baadaea unaweza ukajaribu kwenda kijijini labda huko utafanikiwa, kwa sababu ya laana iliyo juu yako hakika hata kijijini hutafanikiwa.
Kuna watu hukimbilia mijini labda wakidhani huko watafanikiwa lakini kama laana inawasumbua hakika hata waende wapi hawatafanikiwa.
Kumb 28:16 ''Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.''
Dawa ya kuondoa laana sio kuhama eneo bali ni kutubu na kutengeneza kwa KRISTO YESU Mfalme wa uzima.
Unataka kujijua kama una laana?
Kumb 28 itatujibu.
Mtu mwenye laana yuko hivi;
1. Hata ahamie eneo jingine lolote hatafanikiwa.
Kumbu 28:16 ''Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. ''

2. Chanzo chake cha kipato hakimpi faida yeyote.
Kumbu 28:17 '' Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.''

3. Uzao wake unakuwa chini ya laana na pia  Biashara au mradi anaoanzisha hafanikiwi kwa sababu viko chini ya laana
Kumb 28:18 ''Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. ''

4. Kwa kosa la kumkosea MUNGU basi mtu huyo atakuwa mtu wa kuwa na mashaka mashaka, hukemewa, Kudhalilishwa na kutishwa bila kosa kwa sababu ya laana aliyonayo.
Kumbu 28:19-20 '' Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo, BWANA atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.''

5. Kwa Kumkosea MUNGU basi Laana yake inaweza kutengeneza magonjwa mabaya.
Kumbu 28:22 ''BWANA atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa ukaufu, na kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie.''

6. Kufungwa kwa baraka kutoka kwa MUNGU.
Kumb 28:23 ''Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma.''

7. Kwa kumkosea MUNGU basi Mazuri anayoyatarajia yatageuka kuwa mabaya
Kumbu 28:24 '' BWANA  atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie.''

8. Kwa Kumkosea MUNGU basi Adui kwenye ulimwengu wa roho watampiga.
Kumbu 28:25 '' BWANA atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani.''

9. Atakuwa mtu wa kuonewa.
Kumb 28:29 ''  utakwenda kwa kupapasa-papasa mchana, kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika njia zako; nawe sikuzote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.''

10.  Kupata Hasara zisizoisha.
Kumb 28:38-39 '' Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila. Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu.''

11. Wageni au watu wapya wakija wanafanikiwa lakini yeye yuko pale pale, Pia atateswa na madeni
Kumb 28:43-44 '' Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe; yeye atakuwa ni kichwa, wewe utakuwa mkia. ''

12. Akipata mali au pesa wanatokea walaji ili asifanye chochote cha kimaendeleo.
Kumb 28:50-51 ''taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana; naye atakula uzao wa ng'ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa;''

Hizi ni alama chache tu za mtu anayesumbuliwa na laana.
Ndugu yangu ni muhimu kujua kwamba damu ya YESU inaweza kufuta laana zote lakini ni mpaka uombe na sio kujifariji tu.
Kanuni ya laana ni kwamba mkubwa anamlaani mdogo hivyo na kuondoka laana kunahitajika nguvu kubwa kuliko mtoa laana wa kidunia.
Kama laana imetoka kwa MUNGU basi dawa ni kutubu tu kwa MUNGU na kutengeneza njia zako kwa kuanza kutenda yale ayatayo MUNGU.

YESU KRISTO ana uwezo wa kukuweka huru kweli kweli mbali na laana, lakini hadi uamue wewe kuwekwa huru.
Yohana 8:36 '' Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.''

Ewe mteule wa MUNGU nakuomba Mche MUNGU na timiza utakatifu wako kwa kumtii MUNGU hata katika matoleo.
Pia usitumie ulimi wako kulaani watu wa MUNGU bali laani shetani na jeshi lake.
Yakobo 3:9-10 ''Kwa huo(Ulimi) twamhimidi MUNGU  Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa MUNGU. Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.''
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.

MUNGU AKUBARIKI.

HALI YA KIROHO YA ARDHI INAYOHUSIKA NA KUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO sehemu 1.

✨1⃣ *SEMINA YA NENO LA MUNGU DAR ES SALAAM TANGANYIKA PACKERS*

*HALI YA KIROHO YA ARDHI  INAVYOHUSIKA NANKUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO*

*MWL MWAKASEGE*

*DAY 1: 5 MARCH 2017*

Semina hii italenga maeneo  ya ardhi maalumu ya muhimu  yanayohusika kufunga watu  namna ya kuwafungulia.

*LENGO: KUHAKIKISHA MAFANIKIO YAKO YALIYOFUNGWA KATIKA ARDHI YANAFUNGULIWA*.

*1* *KUFUNGUA MAFANIKIO  YAKO YALIYOFUNGWA NA HALI YA KIROHO YA ARDHI INAYOFANYA HALI YA MAHALI UNAPOSIHI PAWE NYUMBA YA UTUMWA*.

_Kumbukumbu la Torati 6 : 12 ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, nyumba ya utumwa._ Kufuatana na 2 Nyakati 7:14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, *na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao*. Nchi maana yake ni ardhi yenye mipaka halali ya kiumiliki

>>Hapa anazungumzia nchi na sio taifa.. maana taifa linahusisha mkusanyiko wa watu walio katika uongozi wa waliokubaliana.Taifa nalo lina mlololongo wake. Katika biblia  kuna taifa.. jamaa kabisa.. jamaa na lugha. Taifa linaweza kuwepo lakini halipo katika nchi yake.. biblia inasema  _Au Mungu amekwenda wakati gani akajitwalia taifa toka kati ya taifa lingine, kwa majaribu, na kwa ishara, na kwa maajabu, na kwa vita, na kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa maogofya makuu, kama vile Bwana, Mungu wenu, alivyowatendea ninyi katika Misri, mbele ya macho yenu? Kumbu 4:34_  . Israel walikuwa taifa lakini walikuwa katika nchi ya Misri.

Wakati unasoma jua namna ya kutofautisha kati ya nchi na taifa, na nilipoanza kulitazama hili suala la ardhi lilinipa kujua  mambo mengi sana. Nilipoanza kufundisha hali ya ardhi katika  mkoa mmoja.. watu walianza kuzunguka na kusema Mwakasege  kapata wapi hiki kitu.. watu wa kule waliniambia na niliwaambia muwe na amani.. maana hili neno ni la Mungu.  Maana si wengi wanajua kuwa haya mambo ninayoongea yapo kwenye biblia.

Huwa nafundisha waalimu kuwa kabla ya kufundisha hilo neno liweke kwenye matendo kwanza wewe mwenyewe maana yake fundisha kwa shuhuda na hapa tutafanya maombi hapa ili mpate kuona. Ukiona nakufundisha masomo haya ujue mimi mwenyewe nimeyaweka kwenye matendo na ndio nimeona matokeo yake na ndipo nakuja kukufundisha kitu halisi ninanchokijua.

*2.UKILINGANISHA 2 NYAKATI 7:14 NA KUMB 6.12 UTAONA  YA KUWA HALI YA KIROHO YA ARDHI INAWEZA GEUZA ENEO KUWA NYUMBA  YA UTUMWA.*

Kumbukumbu la Torati 6 :12 ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, *nyumba ya utumwa*

Nchi ni ardhi yenye mipaka halali na nchi hapa kwa mujibu wa kumbu 6:12.. *nchi ya misri nyumba ya utumwa* kwa hiyo ardhi  ya Misri imefanyika nyumba ya utumwa.Ardhi ina uwezo wa kufanya eneo kuwa nyumba ya utumwa.. tunaenda  sawa sawa?Ukitazama kiroho utaona kiupana ardhi maana hamna nchi iliyojengwa kama nyumba lakini Mungu  anaita nchi ya Misri nyumba ya utumwa.

*3.UTUMWA WA WANA WA ISREAEL ULIKUWA WA KIROHO LAKINO ULIJITOKEZA KATIKA MAISHA YAO YA KILA  SIKU*

Hapa kuna sababu 3

*I) Shida haikuwa kazi.. bali mazingira ya kiroho ya kazi waliyokuwa wanafanya hiyo  kazi*

_Kutoka 1 :11-14  Basi wakaweka wasimamizi juu yao wawatese kwa mizigo yao. Nao wakamjengea Farao miji ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi. 12 Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli. 13 Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli kwa ukali; 14 wakafanya maisha yao kuwa uchungu kwa kazi ngumu; kazi ya chokaa na ya matofali, na kila namna ya kazi ya mashamba; kwa kazi zao zote walizowatumikisha kwa ukali._

Tuangalie kazi walizokuwa wanafanya maana kazi zile walizofanya wakiwa Misri ndizo  hata Kanani walifanya maana walikuwa wanajenga miji ya akiba na majumba. Biblia inasema  wakifanya kazi ngumu, sasa hapa nataka uelewe  si kila kazi ngumu ni utumwa. Maana maeneo yote kama ni kushughukika na chokaa na ujenzi kote walifanya (Kanani na Misiri)  sasa tatizo lilkuwa ni mazingira ya kiroho.

Hata walipomlilia Mungu kwa sababu ya Utumwa. _Kutoka 2 :23 Hata baada ya siku zile nyingi mfalme wa Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa._

Utumwa si kazi bali ni mazingira ya kiroho  yanayitengeneza hali  ya kimaisha, na  yanabana fikra na kuweka mipaka namna Ya kufanya  kazi. Na si wengi  wanajua hili. Utasema kwanini  kwa sababu

*2. WALISHINDWA KUJITOA*.

Maana ingekuwa ni kazi wangeacha.. ni sawa na mtu analalamika kuwa kazi ngumu  na bado yuko kazini nalalamika weeee lakini kazi haachi .. sasa si utoke utafute nyepesi, kuna maana gani kulalamika na kuendelea kubaki mazingira yale yale.

Unaweza ukawa mtumwa katika mazingira ya nyumbani na ni tofauti  na mazingira ya gereza maana mazingira ya nyumbani yanadanganya lakini  bado utumwa ni utumwa haijalishi uko gerezani au nyumbani.

Katika mazingira ya kawaida hawakujua kama wako utumwani.. kama Mungu asingewatangazia kuwa watumwa wasingejua. Maana walipoanza kulia Mungu  aliwaondolea utumwa na hakushughulika na uchungu bali  alishughulika na utumwa..Mzee Yakobo alikufa walimzika Kanani na hamna mtu alibaki kule waliacha kaburi tu. Na wote walirudi Misri, hawakujua kwanini wanarudi Misri, sababu ilikuwa ni ya kiroho zaidi.

*3.ILIBIDI  MUNGU  AWATOE KWA NGUVU*

Kumbukumbu la Torati 7 :8 bali kwa sababu Bwana anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza kiapo chake alichowaapia baba zenu, ndiyo sababu Bwana akawatoa kwa mkono wa nguvu, akawakomboa katika nyumba ya utumwa, katika mkono wa Farao, mfalme wa Misri.  Sio swala la kazi bali yalikuwa ni mazingira ya kiroho. Na ilikuwa  kazi ya kulima, au kutengeneza  matofali lakini ilikuwa ni kazi ya utumwa..

Japo walikuwa wanalima lakini  walikuwa wanaona uchungu.. na hawakujua nini kimewabana.. maana kama kazi ingekuwa utumwa basi kila mtu asingetafuta kazi. Maana kuna baadhi ya wapendwa hawataki kufanya kazi na wanaaza kuhalalisha kwa kutumia mistari ya biblia na kusema kuwa utaishi kwa imani  lakini Biblia inasema asitefanya kazi na asile

*4. WAISHIO NDANI YA NYUMBA WANATAMBULIWA KIROHO KWA KUANGALIA JINA LA MMILIKI WA NYUMBA HIYO.*

_Esta 8 :1-2 1 Siku ile mfalme Ahasuero alimpa malkia Esta nyumba yake Hamani, yule adui ya Wayahudi. Mordekai naye akahudhuria mbele ya mfalme; kwa maana Esta alikuwa amedhihirisha alivyomhusu. 2 Basi mfalme akaivua pete yake, aliyompokonya Hamani, akampa Mordekai. Naye Esta akamweka Mordekai kuwa juu ya mlango wake Hamani._

>>Ukisoma ile sura _Esta 7 :10 Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia._

Sasa ubganisha na Esta 8:1.. Ester alipewa nyumba ya hamani.. Nyumba katika ngazi ya kiroho  inatazamwa tofauti sana.

Naanza kueleza Kumb 6:12 ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, *nyumba ya utumwa* Ondoa misri weka utumwa..  hajailishi uko wapi kama  wewe ni Mmsiri watakujua kuwa wewe ni mtumwa  hata kama uko usa au china.

Na walipokuwa wanabishana  juu ya kuteliwa  kwa  Haruni  kuwa Kuhani wa Mungu, Mungu alisema  walete fimbo kwa ajili ya nyumba moja.. maana kila familia  wana ID (Utambulisho) . Haruni hakuhitaji kuleta fimbo ya watoto  wake, maana fimbo moja tu ilitosha kutambulisha familia yake.

Nyumba ya Yakobo   wana kitambulisho kinacho fanana. Kwa hiyo ukisema nyumba ya Yakobo haijalishi wako wapi ila wanatambulika kama ni watoto wa Yakobo. HAMANI alipokufa alikuwa na alama na alipokufa Hamani Ester ndiye alipewa  mamlaka (yaani adui ndio alipewa madaraka) .. haijalishi wanajipanga kiasi gani kurithi lakini Ester ndiye msimamizi mkuu wa nyumba yao yaani ndiye mwenye sauti. .

Ile Pete  ya Hamani alipewa modekai na alipewa na mamlaka kwenye lango.. na nyumba ile ya Hamani waliobaki wote  waliuwa. Haijalishi  hawako nyumbani  lakini  wako marked kiroho kuwa ni wa nyumba ya Hamani .. haijalishi wayahudi  wako wapi.. walikuwa marked..

Nyumba ya baba yako  kama wamepewa adui zako utapa shida  sana.. maana biblia inasema uzao wako utamiliki malango ya adui

_Mathayo 12 :29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake._

Maana yake nani anayemiliki nyumba na uzao wako.. huwezi wafungua waliofungwa kama hauna nguvu ya kumshika yule aliyewashika au wafungwa

*5.MUNGU ALIWATOA WANA WA ISRAEL  KUTOkA KATIKA  NYUMBA YA UTUMWA KWA KUPITIA  KWENYE MALANGO WA NYUMBA YA UTUMWA*

_Mathayo 12 :29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake._

Alitumia damu ya agano na nchi ya misri kipindi kile ilikuwa ina mazingira ya kitumwa na Mungu  alifuata uzao wa Ibarahim na alienda kuwatoa kwa sababu ya agano.. walikuwa na alama za kiagano, japo walikaa maiaka 400 na utumwani na walikuwa hawasogei kimaisha  lakini Mungu aliwatoa.

Je Mafanikio yako hayasogei  kwa kuwa uko  nyumba ya Misri   ya utumwa nayo imekufunga?

Hata kama ni kwenu ardhi  yenu imekuwa nyumba ya utumwa utapata  shida sana. Ndio maana utaona Kijana  ana akili  lakini  yuko  nyumbani, muda wote anazubaa tu nyumbani, na hatafuti hata kazi yupo yupo tu , na  unashangaa watoto  wa jirani wanasogea ila wako wamekwama kabisa..

Wewe unafikiri ni sawasawa hapa kumbe katika ukoo mna alama ya kuwa ni watumwa, yaani mmefungwa na ndio maana hamsogei  na kama mna agano na Mungu na shetani hata waaachia kirahisi rahisi

Maana unalima kama watu wengine, lakini  wako utumwani  Wana wa Israel  hawakujua na ndio maana waliona uchungu wakati wanafanya kazi, kumbe  sababu  ya mazingira  ya kiroho..

Hata wale wasimamizi walikuwa wanasimamia kwa sababu ya mazingira ya kiroho na waliwatesa sana wana wa Isarel,  ndio maana utaona Mtu anahama nyumba kutoka  nyumba  ya kupanga  kwenda kwenye nyumba yake unakuta hata kazi anachaaaza na anakuwa mvivu

Watu wengi hawajui kwanini Mungu aliwapitiasha wana wa Israel langoni katika  nyimba na hawajui kwanini.  Na alitumia malango na alitunia damu ya Pasaka waliyopaka katika malango.  Watu wako hapa wafungwa asipate  kazi.. na hata nyumbani kwake hatoki  na kakwama hapo yaani kafungwa kabisa

Wengine  wamefungwa kwa kitu cha imani na wapo wapo na asilimia kubwa sana ni vijana wa kiume hawafanyi kazi  na wanafika muda wa kuona lakini ukiwauliza kazi hawana majib u wanasema  katika  mlima wa Bwana inapatikana, msichana anakuuliza hivyo anajua kuwa huyu kijana hajajioanga bado. Sasa ili kukuheshimu anatesema ngoja  nikaliombeee kumbe kakuheshimu tuu na hataki kukuabisha.

Kuna  kitu cha imani kimepita mahali na kina shida.  Ukiwaukiza wako wapi watakueleza jina la nyumba  ya baba yao. Yesu anasema  kanisa ni nyumba  alama ya kiroho kanisa inategemea jina la kanisa.. na wengine   ukiwauliza unasali wapi watakupa jina la Mtumishi  na badala jina la kanisa..

Na ina maana ni alama.. ukisema mimi ni mlutheri ina maana una alama au mpetekoste inaonesha alama yao . Lakini akikuambia jina la mtumishi ina maana alama aliyoweka mtumishi ni kubwa (sina shida au ni vibaya ila nakufundisha tu namna ya kutafsiri haya mambo kiroho kwanza. Pia mwingine ukimuuliza jina la mchungaji wako ni nani unakuta hata hajui, ina maana kuan shida mahali mpaka umesahau jina la mchungaji wako. Kwa sababu umeshindwa kukaa chini ya mchungaji na ndio maana unasahau na jina lake .

Ardhi ni kama computer kubwa, nikakanyaga hapa ardhi inajua huyu mtu ni nani.. Ardhi  ya kule nilikozaliwa inaleta ripoti na ile ya kule ninakoishi nayo inaleta report kwa maana ardhi inatunza kumbukumbu na ndio maana Ukikataliwa mjini utakataliwa na mashambani..

Yesu anapitisha kondoo langoni.. na sio dirishani.. , na ndio maana na wewe uli utoke inabidi upite mlangoni maana wanaopita dirishani ni wezi , sasa naenda kufanya maombi hapa naunganisha ardhi ya hapa na ya huko kwako popote ulipo unapotufuatilia. Weka mikono yako katika magoti yako .

Akani alipokorofisha ardhi ilimeza wote  wa nyumbani mwake, sasa chukulia mmoja hayupo na kawaida ardhi inaambiana ina maana nae kule kule alikokuwa nae alimezwa . ndio maana utakuta ardhi ya kwenu umewafunga na wewe uko mbali na kwenu lakini utaona   pale wenzio wanapochanua wewe unachakae.