Jumatatu, 6 Machi 2017

HALI YA KIROHO YA ARDHI INAYOHUSIKA NA KUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO sehemu 1.

✨1⃣ *SEMINA YA NENO LA MUNGU DAR ES SALAAM TANGANYIKA PACKERS*

*HALI YA KIROHO YA ARDHI  INAVYOHUSIKA NANKUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO*

*MWL MWAKASEGE*

*DAY 1: 5 MARCH 2017*

Semina hii italenga maeneo  ya ardhi maalumu ya muhimu  yanayohusika kufunga watu  namna ya kuwafungulia.

*LENGO: KUHAKIKISHA MAFANIKIO YAKO YALIYOFUNGWA KATIKA ARDHI YANAFUNGULIWA*.

*1* *KUFUNGUA MAFANIKIO  YAKO YALIYOFUNGWA NA HALI YA KIROHO YA ARDHI INAYOFANYA HALI YA MAHALI UNAPOSIHI PAWE NYUMBA YA UTUMWA*.

_Kumbukumbu la Torati 6 : 12 ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, nyumba ya utumwa._ Kufuatana na 2 Nyakati 7:14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, *na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao*. Nchi maana yake ni ardhi yenye mipaka halali ya kiumiliki

>>Hapa anazungumzia nchi na sio taifa.. maana taifa linahusisha mkusanyiko wa watu walio katika uongozi wa waliokubaliana.Taifa nalo lina mlololongo wake. Katika biblia  kuna taifa.. jamaa kabisa.. jamaa na lugha. Taifa linaweza kuwepo lakini halipo katika nchi yake.. biblia inasema  _Au Mungu amekwenda wakati gani akajitwalia taifa toka kati ya taifa lingine, kwa majaribu, na kwa ishara, na kwa maajabu, na kwa vita, na kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa maogofya makuu, kama vile Bwana, Mungu wenu, alivyowatendea ninyi katika Misri, mbele ya macho yenu? Kumbu 4:34_  . Israel walikuwa taifa lakini walikuwa katika nchi ya Misri.

Wakati unasoma jua namna ya kutofautisha kati ya nchi na taifa, na nilipoanza kulitazama hili suala la ardhi lilinipa kujua  mambo mengi sana. Nilipoanza kufundisha hali ya ardhi katika  mkoa mmoja.. watu walianza kuzunguka na kusema Mwakasege  kapata wapi hiki kitu.. watu wa kule waliniambia na niliwaambia muwe na amani.. maana hili neno ni la Mungu.  Maana si wengi wanajua kuwa haya mambo ninayoongea yapo kwenye biblia.

Huwa nafundisha waalimu kuwa kabla ya kufundisha hilo neno liweke kwenye matendo kwanza wewe mwenyewe maana yake fundisha kwa shuhuda na hapa tutafanya maombi hapa ili mpate kuona. Ukiona nakufundisha masomo haya ujue mimi mwenyewe nimeyaweka kwenye matendo na ndio nimeona matokeo yake na ndipo nakuja kukufundisha kitu halisi ninanchokijua.

*2.UKILINGANISHA 2 NYAKATI 7:14 NA KUMB 6.12 UTAONA  YA KUWA HALI YA KIROHO YA ARDHI INAWEZA GEUZA ENEO KUWA NYUMBA  YA UTUMWA.*

Kumbukumbu la Torati 6 :12 ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, *nyumba ya utumwa*

Nchi ni ardhi yenye mipaka halali na nchi hapa kwa mujibu wa kumbu 6:12.. *nchi ya misri nyumba ya utumwa* kwa hiyo ardhi  ya Misri imefanyika nyumba ya utumwa.Ardhi ina uwezo wa kufanya eneo kuwa nyumba ya utumwa.. tunaenda  sawa sawa?Ukitazama kiroho utaona kiupana ardhi maana hamna nchi iliyojengwa kama nyumba lakini Mungu  anaita nchi ya Misri nyumba ya utumwa.

*3.UTUMWA WA WANA WA ISREAEL ULIKUWA WA KIROHO LAKINO ULIJITOKEZA KATIKA MAISHA YAO YA KILA  SIKU*

Hapa kuna sababu 3

*I) Shida haikuwa kazi.. bali mazingira ya kiroho ya kazi waliyokuwa wanafanya hiyo  kazi*

_Kutoka 1 :11-14  Basi wakaweka wasimamizi juu yao wawatese kwa mizigo yao. Nao wakamjengea Farao miji ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi. 12 Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli. 13 Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli kwa ukali; 14 wakafanya maisha yao kuwa uchungu kwa kazi ngumu; kazi ya chokaa na ya matofali, na kila namna ya kazi ya mashamba; kwa kazi zao zote walizowatumikisha kwa ukali._

Tuangalie kazi walizokuwa wanafanya maana kazi zile walizofanya wakiwa Misri ndizo  hata Kanani walifanya maana walikuwa wanajenga miji ya akiba na majumba. Biblia inasema  wakifanya kazi ngumu, sasa hapa nataka uelewe  si kila kazi ngumu ni utumwa. Maana maeneo yote kama ni kushughukika na chokaa na ujenzi kote walifanya (Kanani na Misiri)  sasa tatizo lilkuwa ni mazingira ya kiroho.

Hata walipomlilia Mungu kwa sababu ya Utumwa. _Kutoka 2 :23 Hata baada ya siku zile nyingi mfalme wa Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa._

Utumwa si kazi bali ni mazingira ya kiroho  yanayitengeneza hali  ya kimaisha, na  yanabana fikra na kuweka mipaka namna Ya kufanya  kazi. Na si wengi  wanajua hili. Utasema kwanini  kwa sababu

*2. WALISHINDWA KUJITOA*.

Maana ingekuwa ni kazi wangeacha.. ni sawa na mtu analalamika kuwa kazi ngumu  na bado yuko kazini nalalamika weeee lakini kazi haachi .. sasa si utoke utafute nyepesi, kuna maana gani kulalamika na kuendelea kubaki mazingira yale yale.

Unaweza ukawa mtumwa katika mazingira ya nyumbani na ni tofauti  na mazingira ya gereza maana mazingira ya nyumbani yanadanganya lakini  bado utumwa ni utumwa haijalishi uko gerezani au nyumbani.

Katika mazingira ya kawaida hawakujua kama wako utumwani.. kama Mungu asingewatangazia kuwa watumwa wasingejua. Maana walipoanza kulia Mungu  aliwaondolea utumwa na hakushughulika na uchungu bali  alishughulika na utumwa..Mzee Yakobo alikufa walimzika Kanani na hamna mtu alibaki kule waliacha kaburi tu. Na wote walirudi Misri, hawakujua kwanini wanarudi Misri, sababu ilikuwa ni ya kiroho zaidi.

*3.ILIBIDI  MUNGU  AWATOE KWA NGUVU*

Kumbukumbu la Torati 7 :8 bali kwa sababu Bwana anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza kiapo chake alichowaapia baba zenu, ndiyo sababu Bwana akawatoa kwa mkono wa nguvu, akawakomboa katika nyumba ya utumwa, katika mkono wa Farao, mfalme wa Misri.  Sio swala la kazi bali yalikuwa ni mazingira ya kiroho. Na ilikuwa  kazi ya kulima, au kutengeneza  matofali lakini ilikuwa ni kazi ya utumwa..

Japo walikuwa wanalima lakini  walikuwa wanaona uchungu.. na hawakujua nini kimewabana.. maana kama kazi ingekuwa utumwa basi kila mtu asingetafuta kazi. Maana kuna baadhi ya wapendwa hawataki kufanya kazi na wanaaza kuhalalisha kwa kutumia mistari ya biblia na kusema kuwa utaishi kwa imani  lakini Biblia inasema asitefanya kazi na asile

*4. WAISHIO NDANI YA NYUMBA WANATAMBULIWA KIROHO KWA KUANGALIA JINA LA MMILIKI WA NYUMBA HIYO.*

_Esta 8 :1-2 1 Siku ile mfalme Ahasuero alimpa malkia Esta nyumba yake Hamani, yule adui ya Wayahudi. Mordekai naye akahudhuria mbele ya mfalme; kwa maana Esta alikuwa amedhihirisha alivyomhusu. 2 Basi mfalme akaivua pete yake, aliyompokonya Hamani, akampa Mordekai. Naye Esta akamweka Mordekai kuwa juu ya mlango wake Hamani._

>>Ukisoma ile sura _Esta 7 :10 Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia._

Sasa ubganisha na Esta 8:1.. Ester alipewa nyumba ya hamani.. Nyumba katika ngazi ya kiroho  inatazamwa tofauti sana.

Naanza kueleza Kumb 6:12 ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, *nyumba ya utumwa* Ondoa misri weka utumwa..  hajailishi uko wapi kama  wewe ni Mmsiri watakujua kuwa wewe ni mtumwa  hata kama uko usa au china.

Na walipokuwa wanabishana  juu ya kuteliwa  kwa  Haruni  kuwa Kuhani wa Mungu, Mungu alisema  walete fimbo kwa ajili ya nyumba moja.. maana kila familia  wana ID (Utambulisho) . Haruni hakuhitaji kuleta fimbo ya watoto  wake, maana fimbo moja tu ilitosha kutambulisha familia yake.

Nyumba ya Yakobo   wana kitambulisho kinacho fanana. Kwa hiyo ukisema nyumba ya Yakobo haijalishi wako wapi ila wanatambulika kama ni watoto wa Yakobo. HAMANI alipokufa alikuwa na alama na alipokufa Hamani Ester ndiye alipewa  mamlaka (yaani adui ndio alipewa madaraka) .. haijalishi wanajipanga kiasi gani kurithi lakini Ester ndiye msimamizi mkuu wa nyumba yao yaani ndiye mwenye sauti. .

Ile Pete  ya Hamani alipewa modekai na alipewa na mamlaka kwenye lango.. na nyumba ile ya Hamani waliobaki wote  waliuwa. Haijalishi  hawako nyumbani  lakini  wako marked kiroho kuwa ni wa nyumba ya Hamani .. haijalishi wayahudi  wako wapi.. walikuwa marked..

Nyumba ya baba yako  kama wamepewa adui zako utapa shida  sana.. maana biblia inasema uzao wako utamiliki malango ya adui

_Mathayo 12 :29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake._

Maana yake nani anayemiliki nyumba na uzao wako.. huwezi wafungua waliofungwa kama hauna nguvu ya kumshika yule aliyewashika au wafungwa

*5.MUNGU ALIWATOA WANA WA ISRAEL  KUTOkA KATIKA  NYUMBA YA UTUMWA KWA KUPITIA  KWENYE MALANGO WA NYUMBA YA UTUMWA*

_Mathayo 12 :29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake._

Alitumia damu ya agano na nchi ya misri kipindi kile ilikuwa ina mazingira ya kitumwa na Mungu  alifuata uzao wa Ibarahim na alienda kuwatoa kwa sababu ya agano.. walikuwa na alama za kiagano, japo walikaa maiaka 400 na utumwani na walikuwa hawasogei kimaisha  lakini Mungu aliwatoa.

Je Mafanikio yako hayasogei  kwa kuwa uko  nyumba ya Misri   ya utumwa nayo imekufunga?

Hata kama ni kwenu ardhi  yenu imekuwa nyumba ya utumwa utapata  shida sana. Ndio maana utaona Kijana  ana akili  lakini  yuko  nyumbani, muda wote anazubaa tu nyumbani, na hatafuti hata kazi yupo yupo tu , na  unashangaa watoto  wa jirani wanasogea ila wako wamekwama kabisa..

Wewe unafikiri ni sawasawa hapa kumbe katika ukoo mna alama ya kuwa ni watumwa, yaani mmefungwa na ndio maana hamsogei  na kama mna agano na Mungu na shetani hata waaachia kirahisi rahisi

Maana unalima kama watu wengine, lakini  wako utumwani  Wana wa Israel  hawakujua na ndio maana waliona uchungu wakati wanafanya kazi, kumbe  sababu  ya mazingira  ya kiroho..

Hata wale wasimamizi walikuwa wanasimamia kwa sababu ya mazingira ya kiroho na waliwatesa sana wana wa Isarel,  ndio maana utaona Mtu anahama nyumba kutoka  nyumba  ya kupanga  kwenda kwenye nyumba yake unakuta hata kazi anachaaaza na anakuwa mvivu

Watu wengi hawajui kwanini Mungu aliwapitiasha wana wa Israel langoni katika  nyimba na hawajui kwanini.  Na alitumia malango na alitunia damu ya Pasaka waliyopaka katika malango.  Watu wako hapa wafungwa asipate  kazi.. na hata nyumbani kwake hatoki  na kakwama hapo yaani kafungwa kabisa

Wengine  wamefungwa kwa kitu cha imani na wapo wapo na asilimia kubwa sana ni vijana wa kiume hawafanyi kazi  na wanafika muda wa kuona lakini ukiwauliza kazi hawana majib u wanasema  katika  mlima wa Bwana inapatikana, msichana anakuuliza hivyo anajua kuwa huyu kijana hajajioanga bado. Sasa ili kukuheshimu anatesema ngoja  nikaliombeee kumbe kakuheshimu tuu na hataki kukuabisha.

Kuna  kitu cha imani kimepita mahali na kina shida.  Ukiwaukiza wako wapi watakueleza jina la nyumba  ya baba yao. Yesu anasema  kanisa ni nyumba  alama ya kiroho kanisa inategemea jina la kanisa.. na wengine   ukiwauliza unasali wapi watakupa jina la Mtumishi  na badala jina la kanisa..

Na ina maana ni alama.. ukisema mimi ni mlutheri ina maana una alama au mpetekoste inaonesha alama yao . Lakini akikuambia jina la mtumishi ina maana alama aliyoweka mtumishi ni kubwa (sina shida au ni vibaya ila nakufundisha tu namna ya kutafsiri haya mambo kiroho kwanza. Pia mwingine ukimuuliza jina la mchungaji wako ni nani unakuta hata hajui, ina maana kuan shida mahali mpaka umesahau jina la mchungaji wako. Kwa sababu umeshindwa kukaa chini ya mchungaji na ndio maana unasahau na jina lake .

Ardhi ni kama computer kubwa, nikakanyaga hapa ardhi inajua huyu mtu ni nani.. Ardhi  ya kule nilikozaliwa inaleta ripoti na ile ya kule ninakoishi nayo inaleta report kwa maana ardhi inatunza kumbukumbu na ndio maana Ukikataliwa mjini utakataliwa na mashambani..

Yesu anapitisha kondoo langoni.. na sio dirishani.. , na ndio maana na wewe uli utoke inabidi upite mlangoni maana wanaopita dirishani ni wezi , sasa naenda kufanya maombi hapa naunganisha ardhi ya hapa na ya huko kwako popote ulipo unapotufuatilia. Weka mikono yako katika magoti yako .

Akani alipokorofisha ardhi ilimeza wote  wa nyumbani mwake, sasa chukulia mmoja hayupo na kawaida ardhi inaambiana ina maana nae kule kule alikokuwa nae alimezwa . ndio maana utakuta ardhi ya kwenu umewafunga na wewe uko mbali na kwenu lakini utaona   pale wenzio wanapochanua wewe unachakae.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni