Alhamisi, 13 Julai 2017

Ijumaa, 7 Julai 2017

ROHO MTAKATIFU NI ROHO WA KRISTO.

Ingawa ROHO MTAKATIFU ni nafsi na Mwana, ameunganika na Mwana wala hawezi kutengwa naye, kama vile Mwana na Baba walivyounganika ROHO naye hawezi kutenganika.


Yohana 5

43 Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu, wala ninyi hamnipokei; mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea huyo.

Pia


Yohana 14

26 Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia..


ROHO MTAKATIFU ni Roho wa YESU Kristo. Ana tabia ya Kristo kama vile YESU alivyokuwa na tabia ya Baba (Mdo 16:6-7, Warumi 8:8; Gal 4:6; Flp 1:19; 1Pet 1:11: pia Ebr1:3)


Kwa njia ya ROHO MTAKATIFU, YESU anaendelea kuwa pamoja na Wanafunzi wake, ingawa kimwili hayupo ulimwenguni tena 

(Yoh 14:18  Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.

 Gal 2:20 Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.

Kol 1:27 ambao Mungu alipenda kuwajulisha jinsi ulivyo utajiri wa utukufu wa siri hii katika Mataifa, nao ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu


Katika ROHO MTAKATIFU tunaunganishwa kwa YESU NA KWA MUNGU katika wakati mmoja ambapo auanganishwaye katika hali hiyo huwa yuko katika ulimwengu wa ROHO na si vinginevyo.

Vile vile fikra zake zote haziwi nje ya kuwaza Matendo makuu ya MUNGU katika hali yake. Ndivyo ilivyo katika hali hiyo huwa tabia ya Mwamini inakuwa zaidi na viwango vya kumtafuta MUNGU huwa vya hali ya juu 


ROHO anaitwa Mshauri au Msaidizi kwa sababu anawapa wafuasi wa YESU ushauri na msaada kama vile YESU alivyowapa alipokuwa nao kimwili. Katika njia ya ROHO MTAKATIFU, kuwepo kwa YESU ambako katika karne ya kwanza kulikuwa na kikomo katika Palestina tu, kwa kweli huwa pasipo wakati wa duniani kote (Yn 14:16,18,26; 15:26; 16:7)

Kwa hiyo haiwezekani Kabisakuwa na ROHO MTAKATIFU pasipo kuwa na YESU Kristo. Hali kadhalika haiwezekani kuwa na uhusiano na MUNGU kwa njia ya ROHO, lakini siyo kwa njia ya Kristo (mdo 2:48; Rum 8:9-11). ROHO hajitukuzi mwenyewe juu ya Kristo, kwa sababu kazi YA ROHO ni kuwaongoza watu waje kwa Kristo (Yoh 15:26; 1Kor 12:3)


Hakuna mashindano kati ya ROHO na Kristo, kwa sababu ROHO ni Roho wa Kristo. Kuishi ndani ya Kristo ni kuishi ndani ya ROHO , na kuishi ndani ya ROHO ni kuishi ndani ya Kristo (Rum 8:1,9: 2Kor 3:14-18). Kama vile YESU Kristo alivyopokea mamlaka yake kutoka kwa Baba, alivyomtukutuza Baba, vivyo hivyo ROHO hupokea mamlaka yake kutoka kwa Kristo, humtukuza Kristo na huwafundisha watu mambo ya Kristo (linganisha Yoh 8:  28 Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo.

  na 

16:13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.


pia 


Yoh 17:4 Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.

na 16:14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.


pia


 Yoh 17:8 Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.

 na Yoh 14:26 Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.

16:15 Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari.






MUNGU AWABARIKI


Jumatatu, 26 Juni 2017

BIBLIA INAVYOSEMA JUU YA KUINUKA KWA UISLAM.

BIBLIA INAVYOSEMA JUU YA KUINUKA KWA UISLAM:

1 Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.

2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni.

3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi.

4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao.

Ufunuo wa Yohana 9:1-4

Hapa dini mpya inaoneshwa, ikiwa na baadhi ya mafundisho mazuri, NI NYOTA ILIYOANGUKA KUTOKA MBINGUNI, lakini ilikuwa imechanganyikana na MAFUNDISHO MACHAFU, moshi kutoka lile, "SHIMO LA KUZIMU"

Uislam ulianza kwa kulaani uovu wa ibada ya sanamu iliyokuwa inaendeshwa na kanisa la Roman Catholic, (NA HAPA ULIKUWA SAWA).

Kwa hakika kuna Mungu mmoja, na hakuna astahiliye kuabudiwa isipokuwa yeye. Lakini mafundisho ya Uislam yaliyokuwa yanahitajika kwa kanisa asi, YALILETA "MOSHI" KATIKA ULIMWENGU.

"SHIMO LA KUZIMU" katika kiyunani lina maana ya JANGWA au NYIKA yoyote iliyo ukiwa, na hivyo linafaa kabisa KUWAKILISHA JANGWA LA ARABUNI walikotokea wavamizi Waislam wa Kiarabu, KATIKA WINGI UNAOFANANA NA NZIGE.

Abyssos ni neno la Kiyunani linalomaanisha, "SHIMO LA KUZIMU"
na hilo ndilo linalotupatia neno la sasa la kiingereza, linalomaanisha KUZIMU. Waandishi wa kisasa wa Kiislam wanalitumia neno hilo kuielezea jamii ya Kiarabu alikotokea Muhammad: ARABIA@SHIMO LA GIZA.

Katika enzi hizo za ujinga uliokithiri, kulikuwa na eneo ambalo giza zito tena totoro lilikuwa limetuwama... ARABIA... Nalo lilikuwa pweke likiwa limetengwa na bahari kubwa sana ya mchanga. Wafanya biashara wa Kiarabu walikuwa wanasafiri mwendo mrefu kwa kujikokota wala hawakupata punje yoyote ya maarifa katika safari zao. Katika nchi yao hawakuwa na taasisi yoyote ya elimu wala maktaba. Hakuna aliyekuwa anaonekana kuwa na shauku ya kukuza ama kuendeleza elimu... Fikra zao zilikuwa zimejaa miiko, akili na jadi yao ilikuwa ni unyama na ukatili mkubwa, maadili na ufahamu wao vilikuwa vya kishenzi na visivyo staha.

"...Hakukuwa na sheria isipokuwa ile ya ukatili. Uporaji, mashambulizi na mauaji ya watu dhaifu wasio na hatia ilikuwa ndio kawaida... Tukio lolote dogo lilikuwa linaweza kusababisha vita kulipuka kwa hasira za kikatili...
Dhana yoyote waliyokuwa nayo juu ya maadili, utamaduni, na ustaarabu vilikuwa vinaonekana vya kizamani na ushenzi... Walikuwa wakiabudu mawe, miti, sanamu, nyota na mizimu, na kiufupi walikuwa wanaabudu chochote walichokuwa wanakifikria isipokuwa MUNGU.
(Rejea ABDUL A'LAMAUDUDI TOWARDS UNDERSTANDING ISLAM, UK. 41, 42, NAIROBI: THE ISLAMIC FOUNDATION, QUR'AN HOUSE 1973)

Siku moja mfalme Chosroes II wa Uajemi alipokea barua kutoka kwa raia mmoja wa Maka asiyefahamika, ikimtaka amtambue Muhammad kuwa ni nabii wa Mungu. Mfalme aliichana ile barua kwa dharau na akakataa madai ya nabii. Yeye hakujua kuwa, mapema, yeye mwenyewe ataangamia kabisa na ufalme wake pia kuangamizwa, NA KWAMBA NABII HUYU WA AJABU KUTOKA MAKA ANGETAWALA ULIMWENGU. Kuanguka kwa mfalme Chosroes kunafikriwa na wengine kuwa kulikuwa ndio, "UFUNGUO WA SHIMO LA KUZIMU", kwa sababu Muhammad asingeweza kuinuka katika kutawala isipokuwa kwa kuuangusha kwanza ufalme wa Waajemi.

NDIPO WAISLAM WA ZAMANI (SARACENS) KUTOKA UARABUNI, "WAKAPEWA NGUVU", NA KUONGEZEKA SANA MPAKA WAKAWA WENGI MNO KAMA NZIGE.

Bila ya kuwa na dhana ya kitabu cha Ufunuo akilini mwake, mwandishi mmoja alisema hivi juu ya hawa wafuasi wa Muhammad kuwa, " Wa-Osmanlis walisongamana kama NZIGE pande zote, na hakuna kijiji ambacho hakikuwafahamu, mpaka hata kuta za Constantinople". Kama vile nge anavyogonga, ndivyo walivyolipiza kisasi kwa ukatili katika vita.

Muhammad alipokufa, alirithiwa na Abubakari katika mwaka wa 632 B.K, ambaye aliwakusanya makabila ya kiarabu ili kufanya vita. Aliwaamuru wafuasi wake kuheshimu imani za watu wale waliokuwa wanazishika kwa uaminifu amri za Mungu. Ilikuwa inawapasa watu wake kuwaadhibu wale tu waliokuwa wanaabudu sanamu.

Akiwaamuru askari wake: "MSIUCHAFUE USHINDI WENU KWA DAMU ZA WANAWAKE NA AU WATOTO. MSIHARIBU MITENDE, WALA KUCHOMA MASHAMBA YO YOTE YA NAFAKA. MSIKATE MITI YO YOTE YA MATUNDA, WALA KUFANYA UHARIBIFU JUU YA MIFUGO, ISIPOKUWA WALE MTAKAOWAUA KWA CHAKULA.

Kadiri mtakavyoendelea mtawakuta baadhi ya watawa ambao wamejitenga na kuishi katika nyumba za watawa, wakiazimia wenyewe kumtumikia Mungu hivyo, MSIWASUMBUE NA WALA MSIWAUE WALA KUANGAMIZA MAKAZI YAO, na mtakuta aina ya watu wengine walio wa sinagogi la shetani, walionyoa utosi wao, hakikisheni mnapasua vichwa vyao, na msiwape nafasi mpaka ama wamegeuka kuwa Waislam au walipe " ushuru".

Ni watu gani waliokuwa na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao ambao askari wa Abubakari waliamuriwa kuwaacha?

Katika historia yote kumekuwa na waaminifu waliokuwa wanatunza Sabato ya kweli ya Bwana, ambayo ndiyo, "MUHURI YA MUNGU"

Katika siku za Muhammad na Abubakari kulikuwa na waaminifu kama hao. Inaonekana kuwa mwenye mamlaka kuu kuliko Muhammad watu wake waaminifu walindwe!
Waarabu walitumia mno Farasi katika vita vyao. Na "TAJI" inaweza kuwa kilemba, ambacho kwa muda mrefu kilikuwa ni kilemba cha taifa la Waarabu.
Askari walikuwa na nywele ndefu.

Mafungu 5-11

5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu.

6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.

7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu.

8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.

9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani.

10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao.

11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani analo jina lake Apolioni.

Ufunuo wa Yohana 9 :5-11

Hapa tunalo jaribio juu ya usahihi wa unabii na kutimilika kwake kihistoria.

KATIKA UNABII WA BIBLIA SIKU MOJA NI MFANO WA MWAKA MMOJA, (Tazama maelezo ya sura 2:10). Kuna siku 30 katika mwezi wa unabii wa Biblia (linganisha mwanzo 7:11, 8:4 na 7:24 na pia linganisha miezi 42 ya Ufunuo 11:2 na siku 1260 za 11:3 na 12:6). Hivyo "MIEZI MITANO" ya kipindi cha unabii ni sawasawa na miaka 150.

Waislam hawa wa zamani, (SARACENS) "WALIPEWA AMRI", kuutesa " UTAWALA WA KIRUMI WA MASHARIKI KWA MIAKA HII 150, lakini siyo "KUWAUA", yaani siyo KUWASHINDA. Miaka 150 inapasa kuanzia wakati ule, " WATAKAPOKUWA NA MFALME WAO".

Kitabu cha Mithali kinasema, "NZIGE HAWANA MFALME, LAKINI HUENDA WOTE PAMOJA VIKOSI VIKOSI"
Mithali 30:27

Lakini, "NZIGE" wa Waislam, wavamizi walipangwa vizuri sana katika kazi ya kuangamiza, maana walikuwa na mtawala waliyekuwa wanafuata amri zake. Kwa mamia ya miaka baada ya kifo cha Muhammad, wafuasi wake waligawanyika katika makundi mbalimbali hasimu bila ya utawala wowote au mfalme. Lakini karibu na mwisho wa karne ya 13, Othman alianzisha na kuimarisha serikali iliyokuwa inajulikana kama ufalme wa Ottoman (Ufalme wa Kituruki).

"MALAIKA WA SHIMO LA KUZIMU" anaitwa "MALAIKA" katika fasili ya neno la kiyunani ambalo pia linamaanisha "MJUMBE" au "MHUDUMU". Sultani akawa mkuu wa dini ya Kiislam. Jina kwa Kiebrania "ABADONI", na kwa Kiyunani "APOLIONI" lina maana ya "YEYE AANGAMIZAYE". Hivyo ndivyo ilivyokuwa tabia ya watawala wa Kituruki (Ottoman).

Tunajiuliza ni lini Othman, kama mfalme wa kwanza wa Waislam alipofanya mashambulizi yake ya kwanza, "KUUTESA" ulimwengu wa kiistarabu wa Ufalme wa Mashariki?

Edward Gibbon, mtu ambaye aliandika historia lakini hakuamini katika Biblia, ametuachia tarehe ya usahihi zaidi kuwa Julai 27, 1299, ndiyo Othman alifanya mashambulizi yake ya kwanza juu ya Nicomedia.

Gibbon anasema kuwa, "USAHIHI" wa ajabu unaonekana kudhihirisha njozi fulani ya mbio na ukuzi wa uharibifu wa ubwana (Ufalme wa Kituruki).

Tunauliza tena. Je Waturuki "walitesa" ufalme wa Rumi wa Mashariki kwa miaka 150?  Ndiyo, historia inatuambia kuwa waliendeleza vita kuusumbua na kuutes ufalme huo tangu mwaka 1299 mpaka 1449 kwa miaka 150 kamili bila kuuteka kabisa. Halafu badiliko kuu lilitokea. Wafalme wa Rumi ya Mashariki waliendelea kudhoofika na kuwa wapotovu zaidi mpaka ikawa dhahiri kwa kila mtu kwamba muda kitambo wangepoteza uhuru wao.

Wakati mfalme Yohana alipofariki taehe 31 Oktoba, 1448, ndugu zake kwa unyenyekevu, ndugu zake waliomba idhini kwa Sultani wa Uturuki, Murad II, ili kumchagua ndugu yao mkubwa kutawazwa kama mfalme mpya katika mwezi Januari, 1449. Hivyo kwa kumnyenyekea Sultani wa Uturuki, walikiri kuwa uhuru wao ulikuwa umefikia mwisho. Kumbuka kuwa maelezo haya ni ya maana na yaliyo wazi kabisa.

Mafungu 12-15

12 Ole wa kwanza umekwisha pita. Tazama, bado ziko ole mbili, zinakuja baadaye.

13 Malaika wa sita akapiga baragumu, nikasikia sauti moja iliyotoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyo mbele za Mungu,

14 ikimwambia yule malaika wa sita aliyekuwa na baragumu, Wafungue nao malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Frati.

15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu.

Ufunuo wa Yohana 9 :12-15

Ule "OLE WA KWANZA" ilikuwa ni kuinuka kwa nguvu ya Uislam. Baadaye ilikuwa ufuate "OLE WA PILI", na kuwa taabu kuu katika Ulaya. (Sura 11:14). Na "OLE WA TATU" ulikuwa uwe hasira ya kuogofya ya mataifa, pamoja na ghadhabu ya hukumu ya Mungu, itayoleta mwisho wa historia ya ulimwengu wetu (sura ya 11:18).

Katika mwaka 1449, "MALAIKA WA SITA" alifungulia kizuizi kilichokuwa kimewazuia Waislam kuuteka ufalme wa mashariki uliokuwa wenye utajiri na nguvu. Wale "MALAIKA WANNE WALIOFUNGWA KWENYE MTO MKUBWA FRATI" NI KIELELEZO KINACHOTAJA MAJIMBO MANNE TOFAUTI YA WAISLAMU YA ALEPPO, IKONIO, DAMESKI, NA BAGHDAD.

Na hivyo njia ilifunguliwa kwa Sultani ili baadaye aendeshe vita vya ushindi dhidi ya Ulaya. Mji wa Constantinople (sasa Istanbul) ulitekwa na majeshi ya Uturuki katika mwaka 1453.

Lakini zingatia hili: Miaka 150 ilipotimia katika mwaka 1449, uhuru wa mfalme wa Ulaya ulipotezwa siyo kwa mapigano, bali kwa mfalme kuusalimisha kwa hiari uhuru wao mikononi mwa Waturuki. Maana yake alisema. "SIWEZI KUTAWALA MPAKA KWANZA MRUHUSU". Kumbuka kwamba, kadiri tunavyosonga mbele, karibu utaona jambo muhimu mno.

Je ni kwa muda gani ufalme wa Waturuki Waislam ungeendelea kutawala kwa uhuru?

"Mwaka" mmoja wa siku 360 ni miaka halisi 360

Mwezi mmoja wa siku 30 ni miaka 30

Siku moja ya saa 24 ni mwaka 1

Saa 1/24 ya mwaka X 360 ni sawa na siku halisi 15

Jumla tutapata miaka 391 na siku 15

Ni lini hiki kipindi cha miaka 391 na siku 15 kilipoanza?

Ni dhahiri kuwa ni baada ya mwisho wa miaka 150 Waislam walipokoma "KUTESA" ufalme wa Mashariki maana waliutwaa. Baada ya kuongeza hiyo miaka 150 katika tarehe yetu ya kuanzia ya Julai 27, 1299, ni wazi kuwa tutafikia julai 27, 1499. Halafu ikiwa tutaongeza miaka 391 katika julai 27, 1499 tunafikia julai 27, 1840  Kisha ni lazima tuongeze siku nyingine 15.

Tunapata nini kama jibu kamili na la mwisho? Julai 27 ukiongeza siku 15 inapatikana Agost 11, 1840.

Je, Sultani wa Uturuki alipoteza Uhuru wake katika siku hiyo hasa kwa kujisalimisha kwa unyenyekevu na kwa hiari yake kwa watawala wa Ulaya kwa namna ile ile mfalme wa Rumi Mashariki alivyopoteza uhuru wake kwa Sultani mwaka 1449? Tutaona baadaye.

Ikiwa historia itasema ndiyo kwa swali hilo, tutakuwa na ushahidi wa hakika na kustaajabisha kwa mambo mawili:
Kwanza, kwamba utaratibu wa mwaka kwa siku wa kufasili unabii wa Biblia ni sahihi kabisa, na pili, kwamba kidole cha kuogofya cha Mungu kinaelekeza kwa jambo fulani pana na lenye maana kuliko kujifunza juu ya kuinuka na kuanguka kwa falme:

Kitabu cha Ufunuo ndio ufunguo Mungu aliotupatia kufungulia siri ya hukumu yake juu ya ulimwengu wetu wa siku hizi ulio mkaidi.

Pale msomaji asiyejali anapokuwa haoni kitu bali tu jangwa lisilofaa, katika kitabu cha Ufunuo sisi tunapata utajiri uliofichwa na wenye maana kubwa mno kwa watu wa Mungu. Kitambo kidogo tutaona ni nini historia inasema kilichotokea siku ya Agosti 11, 1840.

Kwanza, hebu na tuangalie kwa muda tu vipi Yohana anaelezea namna majeshi ya Kiislamu ya Uturuki yalivyowahi kutia hofu mataifa ya Ulaya kwa karne nyingi:

*Linganisha Maandiko Matakatifu yanavyouhesabu wakati katika UFUNUO 13:5, 12:6,14. Ni dhahiri kuwa "mwaka" wa Biblia ni siku 360 na "mwezi" wa Biblia ni siku 30.

Mafungu 16-19

16 Na hesabu ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa elfu ishirini mara elfu kumi; nilisikia hesabu yao.

17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti.

18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao.

19 Kwa maana nguvu za hao farasi ni katika vinywa vyao, na katika mikia yao; maana mikia yao ni mfano wa nyoka, ina vichwa, nao wanadhuru kwa hivyo.

Ufunuo wa Yohana 9:16-19

HAPA KUNATAJWA MATUMIZI YA BARUTI KWA MARA YA KWANZA KATIKA HISTORIA YA MWANADAMU.

Kwa Yohana, ambaye kwa kweli hakuwahi kuona bunduki au baruti, mashujaa wa Kiislam wakiwa wamepanda farasi wakipiga bunduki zao wataonekana katika upeo wa macho yake kana kwamba, "KATIKA VINYWA VYAO HUTOKA MOTO NA MOSHI NA KIBERITI"

Mpaka mwaka 1453 B.K. kuta za mji wa Constantinople zilikuwa zimestahimili mashambulizi ya majeshi mengi, na hivyo ufalme ulikuwa umeokoka na hatari. Lakini sasa Waturuki wa Ottoman wakatumia kwa mara ya kwanza mizinga mipya na mikubwa pamoja na baruti katika kubomoa zile kuta zilizokuwa hapo awali haziingiliki. Kutumiwa kwa baruti na mizinga kulimaliza ulinzi wa mwisho wa jeuri ya ufalme wa zamani wa Warumi. Ubinafsi na ubadhirifu ulikuwa umeangamiza ustaarabu wa zamani.

Lakini sasa katika mwaka 1840, ubinafsi na ubadhirifu ulikuwa umepoozesha jeuri ya utawala wa Kiislam katika mwaka 1838, vita vikali vililipuka kati ya masultani wa Uturuki na Misri, Misri ikiwa mshindi.

Katika mwaka 1840, mataifa yenye nguvu manne ya Ulaya yaliingilia kati kwa kuhofia kwamba Misri ingeweza kwa muda mfupi kuchukua kiti cha enzi cha Sultani wa Uturuki katika kuhangaika kwake. Sultani ambaye alikuwa amedhoofishwa kwa hiari ALISALIMISHA UHURU WAKE MIKONONI MWA HAYA MATAIFA MANNE YA ULAYA, akiwaachia kumwendeshea mambo yake. Alimtuma mjumbe wake kwenda kwa mtawala wa Misri kutoa ujumbe kutoka kwa Mataifa manne ya Ulaya, ujumbe ulioweka mikononi mwao mambo yake.

Ilikuwa ni Agosti 11, 1840, ndiyo huyo mjumbe alipowasili Alexandria, na siku hiyo alikabidhi ujumbe mikononi mwa mtawala wa Misri.

Katika siku hiyo, uhuru wa Sultani ulikuwa wapi? ULIKUWA UMETOWEKA! Na "tangu siku hiyo. Uturuki ya Kiislamu imebakia tu kwa ruhusa na kutegemea kuungwa mkono na mataifa ya Ulaya".

Jambo hili lilipofahamika kwa umati wa wapenda Biblia walisadiki usahihi wa kanuni ya mwaka kwa siku ya kufasili unabii wa Biblia. Kilichoonekana kuwa si jambo la muhimu kihistoria kilitoa kwa dhati ushahidi wa kuridhisha kuwa vitabu vya Danieli na Ufunuo viliandikwa kwa uongozi wa Mungu, na vinatoa ujumbe muhimu sana kwa wakazi wa dunia ya sasa.

Wanazuoni na watafiti wa leo wanaweza kutofautiana katika kuhesabu wakati kipindi hiki cha miaka 391 kilipoanza na kumalizika. Jambo la kushangaza ni kwamba matukio makuu ya historia ndefu ya himaya ya Ottoman yanasimuliwa kwa usahihi kabla hayajatukia katika unabii. Kama tulivyoona katika Danieli mwitikio wa historia ni kama jiwe lililovunjwa linaloweza kurudishwa lilivyokuwa. Wapagani wengi waliongoka miaka ya 1840 kwa kushuhudia kutimizwa kwa unabii unaofuata kanuni ya MWAKA-SIKU na imani watu mamilioni wasiojulikana wamekuwa wakitiwa nguvu na unabii huu. Kwa hakika ndiye BWANA aliyekuwa ameutoa.

Mafungu 20, 21

20 Na wanadamu waliosalia, wasiouawa kwa mapigo hayo, hawakuzitubia zile kazi za mikono yao, hata wasiwasujudie mashetani, na sanamu za dhahabu na za fedha na za shaba na za mawe na za miti, zisizoweza kuona wala kusikia wala kuenenda.

21 Wala hawakuutubia uuaji wao, wala uchawi wao, wala uasherati wao, wala wivi wao.

Ufunuo wa Yohana 9:20-21

Ingawa makundi ya Waislamu yaliachwa huru juu ya ulimwengu wa Kikristo ulioasi, watu walikataa kujifunza somo la toba. Kwa hiyo tunaona kuwa Mungu huwa anaruhusu, "OLE" kuujia ulimwengu ili kuwafanya wenye dhambi kuzinduka, na kuwaongoza kuiendea toba. Ole baada ya ole zilifuatana, lakini bado wanadamu walikuwa wanazipenda dhambi zao. Je, "OLE WA TATU" utawaongoza kwenye toba? Wakati ule utakapofika, watakuwa wamechelewa mno!

Mpendwa unayesoma, Je, utajitoa moyo wako kwa toba leo?

*MSOMAJI AMBAYE ANGEPENDA KUONA DONDOO KUTOKA KWA MAGAZETI YA AGOSTI NA SEPTEMBA, 1840, YAKITOA MAELEZO KAMILI JUU YA MATUKIO YA AGOSTI 11, 1840, ANAWEZA KUANGALIA KATIKA KITABU CHA, "DANIEL AND THE REVELATION", KILICHOANDIKWA NA URIAH SMITH, KURASA 513-516.

MUNGU AWABARIKI

Jumatano, 10 Mei 2017

MOYO WA MTU HUAMBATANA NA MUNGU AU MALI.

MOYO WAKO UMEAMBATANA NA MUNGU AU MALI

HALELUYA

Mathayo 19;16~24

16 Na tazama mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu nitende jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?
17 Kwani kuniuliza habari ya wema? Alieye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima zishike amri
18 Akamwambia zipi? Yesu akasema, Ni hizi usiue,usizini,usiibe,usishuhudie uongo,
19 Waheshimu baba yako na mama yako na mpende jirani yako kama nafsi yako.
20 Yule kijana akamwambia, haya yote nimeyashika nimepungukiwa na nini tena?
21 Yesu akamwambia ukitaka kuwa mkamilifu enenda ukauze ulivyo navyo uwape masikini nawe utakuwa na hazina mbinguni kisha njoo unifuate
22 Yule kijana alipo sikia neno lile akaenda zake kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Yesu akawaambia wanafunzi wake amini nawaambieni ya kwamba itakuwa shida tajili kuingia katika ufalme wa Mbinguni
24 *Nawaambia tena ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu*

Bwana Yesu apewe sifa sana

Tumesoma habari ya yule kijana tajiri anamuuliza Yesu kwamba afanye nn aulithi ufalme wa mbinguni. Kijana alipenda kwenda mbinguni na ndio maana anamuuliza Yesu kwamba afanye nn ili aingie mbinguni Yesu anamuuliza kama anazijua amri kijana alimjibu kuwa yote ameyashika na anayafanya sasa kwa kuwa alikuwa na shauku ya kutaka kuingia mbinguni anamuuliza nimepungukiwa nn tena kama ni amri anazijua na anayafanya ingekuwa ni mtu mwingine ingewezekana kwa kuwa Yesu amemwambia amri na anazijua angeishia hapo kuuliza angesha jua mbingu yangu lkn kijana akawa na shauku ili ajua labda kama amepungukiwa kitu kisimfanye aende mbinguni na Yesu ndipo anamjibu na Yesu aliijua shauku ya kijana na aliona kabisa huyu anapenda kwenda mbinguni na alijua pamoja na kijana kutaka kwenda mbinguni yulr kijana moyo wake ulikuwa haujashikamana na nae ila umeshikamana na mali ndipo anamwambia kauze vyote ulivyo navyo ukawape maskin kisha unifuate. Kijana aliondoka kwa huzuni sababu moyo wake ulikuwa kwenye mali na sio Mungu na ndio maana jibu la Yesu lilimfadhaisha sana. Ni kweli kijana alitaka kwenda mbingun lkn moyo haukuwa na Mungu bali mali
Yesu alipo kuwa anamwambia kijana akauze mali zake hakuwa na maana amfilisi ila alitaka kujua kama kweli moyo wake umeshikamana naye

Mpendwa Mungu anapo tuambia tumtolee sadaka si kwamba amataka pesa zetu sababu vyote ni mali yake anataka kupima mioyo yetu kama kweli tunampenda Mungu na kujitoa hata kwa mali kwa ajili yake. Na ndio maana anasema tutoe kwa hiyari yaan mioyo ya kupenda lkn pia maandiko yanasema hazina na mtu ilipo na moyo wake ulipo inamaana ww ukitoa kasehemu kadogo ka mali zako ndio kaupendo kako kalivyo kwa Mungu

Hebu tusome mf huu kwa baba yetu Ibrahimu tuone jinsi sadaka ilivyo na nguvu na Mungu jinsi anavyo tupima

Mwanzo 22;1~12
Hapa tunasoma habari za Ibrahimu. Mungu alimjaribu akamwambia amtoe sadaka mwanae wa pekee si kwamba Mungu alikuwa akimtaka Isaka na si kwamba Mungu alikuwa hajui kama Ibraimu hamchi yeye ila alimjaribu kuupima moyo wake kama kweli Ibrahimu anampenda Mungu kwa moyo wake na Mungu alithibitisha hilo kwamba kweli.Ibrahimu anampenda kwa maana hakumzuilia mwanae wa pekee alitaka kumchinja soma mstr wa 12

Hivyo mpendwa Mungu akikusemesha kwa habar ya kutoa hata kiwe kitu muhimu vip kwako toa sababu Mungu haitaji hicho anahitaji ule utayari wako wa kujitoa kwa moyo kwa ajili yako.

Je moyo wako.umeshikamana na nani Mungu au mali au kazi kama ni Mungu jipime unavyo jitoa kwa ajili ya Mungu ile kwa mali au muda hicho ndicho kitakacho kuthibitishia unampenda Mungu hebu muangalie mama mjane alitoa senti mbili lkn Yesu alimuona ametoa kuliko wote sababu hakutoa sehemu ya mali bali alitoa kwa moyo tena chote alicho nacho Mungu.anaangalia moyo wako unavyo jitoa angalii kiasi unachotoa na moyo ndio kipimo cha ww unampenda Mungu

kijana alishindwa kuendelea na Yesu sababu alikuwa na mali nyingi sana na moyo wake ulikuwa kwenye mali alizo nazo sio kwa Yesu

Je ww moyo wako uko wapi?
Je unampenda Mungu kweli?
Je unajitoa kiasi gani kwa ajili ya Mungu

Ibrahimu Mungu alipo uona moyo wake kwamba anamcha Mungu akumzuilia mwana wake wa pekee Mungu alimbariki Ibrahimu alitengeneza agano nae mpaka leo watu tujajibarikia katika uzao wake taifa la Israeli

SADAKA YAKO IAMBATANE NA MOYO WAKO NA MOYO WAKO UAMBATANE NA BWANA SI MALI.

Amosi 3;3 je! watu wawili waweza kutembea pamoja wasipokuwa wamepatana?
Hauwezi kutembea na mtu pasipo kupatana naye. Namaanisha Huwezi kutembea na Mungu au kuwa karibu na Mungu wakati moyo wako upo mbali nae na moyo wako kuwa karibu nae ni vile unavyo jitoa kwa ajili yake(MUNGU)  na kutembea katika sheria zake.

ROHO MTAKATIFU aendelee kukufundisha.

Barikiwa .

Jumanne, 2 Mei 2017

JE, YESU KRISTO NA MUHAMMAD WALITUMWA NA MUNGU MMOJA?

Kumekuwa na hoja moja ambayo inasumbua vichwa vya watu wengi.
Je, YESU NA MUHAMMADCWALITUMWA NA MUNGU MMOJA?
Leo nakata utepe kwa kutumia BIBLIA na Quran. Tunapaswa kuangalia hoja moja ya msingi, je kauli zao zinafanana? au zinapingana? Kama hazifanani yakupasa ujiulize mara mbili mbili, kati ya Moja na Mbili ipi iliabza kujitambulisha na ipi ilikanusha utambulisho.
Muhammad alizaliwa mwaka 570 bk,
Wakati anazaliwa aliikuta kauli hii
Mathayo : Mlango 3
17 na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.
Pia andiko hili alilikuta, ambalo ni KAULI YA MALAIKA
Luka : Mlango 1
32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
Hoja ya msingi ni kwamba, Je Malaika aliyetumwa na Mungu kusema kauli hii, ndiye aliyetumwa tena kupinga kauli tangulizi?
Lazima tujiulize kuhusu hili.
Tazama Quran 2:116
116.
Na ati wanasema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu! Ametakasika na hayo. Bali vyote viliomo mbinguni na duniani ni vyake. Vyote vinamt'ii Yeye.
Hii kauli ilikuja kupinga kauli inayopatikana kwenye LUKA 1:30-37
Ambayo inasema

Luka 1:
30. Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.
34 Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?
35 Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.
36 Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa;
37 kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.



Watu wote Wanajua kuwa MUNGU hawezi kujipinga atamkapo.

Hapo tu unapata picha kuwa, Wawili hawa walitoa ujumbe sehemu mbili tofauti.

Ukisoma Biblia iliyotangulia kuleta huu ujumbe juu ya YESU KUITWA MWANA WA MUNGU miaka 600 kabla ya kushuka aya zilizo kanusha ujumbe wa mwanzo.


Hapa yatupasa kuwa makini.


Tazama Quran 4:171


171.
Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu, wala msimseme Mwenyezi Mungu ila kwa lilio kweli. Hakika Masihi Isa mwana wa Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na neno lake tu alilo mpelekea Maryamu, na ni roho iliyo toka kwake. Basi Muaminini Mwenyezi Mungu na Mitume wake. Wala msiseme: Utatu. Komeni! Itakuwa kheri kwenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja tu. Ametukuka Yeye na kuwa na mwana. Ni vyake Yeye vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mtegemewa wa kutosha.

Hii aya inapinga Maneno ya YESU yanayopatikana katika 

 YOHANA 9:35-37 inasema hivi


35 Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu?
36 Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini?
37 Yesu akamwambia, Umemwona, naye anayesema nawe ndiye.
38 Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia.
39 Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.


Hapa kuna habari kuhusu vipofu wa kiroho, ambapo YESU anathibitisha kuwa ANAPASWA KUAMINIWA KUWA NDIYE MWANA WA MUNGU.

Kumbuka aya zinasema kuwa YESU HAKUFANYA DHAMBI HATA SIKU MOJA, 

Hivyo  kitendo cha Muhammad kusema kuwa YESU SI MWANA WA MUNGU NI Kumaanishi kuwa YESU ni mwongo baada ya kujiita MWANA WA MUNGU.



Na kama 
ni hivyo inamjumlisha na MALAIKA aliyrtumwa na MUNGU, pia MUNGU aliyemtuma MALAIKA + YESU WOTE NI WAONGO, HILI HALIKUBARIKI. Maana Aya zinasema YESU hakutenda dhambi na ujumbe wake hauwezi kuwa wa UONGO bali KWELI YAKE INABAKI KUWA KWELI MILELE YOTE.




Kwa mujibu wa Quran inaonyesha kuwa mwongo kwa kujiita MWANA WA MUNGU.
Hapa unapata jibu kuwa YESU na Muhammad walitumw na Miungu tofauti kulingana na maneno yao.


YESU ALIKIRI KWA KINYWA CHAKA PALE ALISEMA


YESU alisema anapaa kwenda kwa Baba yake, ambaye ni Mungu wake pia ni Baba yetu, pia Mungu wetu.



HUYU MUNGU ALIYE MTUMA YESU YEYE NI BABA WA WOTE,


Ila huyu aliyemtuma Muhammad hakubaliani na jambo hili na anadai kuwa inakaribia mbingu na ardhi kutatuka kisa Kuitwa Baba, yaana ukisema kuwa YESU ni Mwana wa Allah umeleta mtafaruku mkubwa.

Kwa ushahidi soma aya hii kutoka kwenye Quran 👇👇

Quran 19:

88.
Na wao ati husema kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana!
89.
Hakika mmeleta jambo la kuchusha mno!
90.
Zinakaribia mbingu kutatuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande.
91.
Kwa kudai kwao kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana.
92.
Wala hahitajii Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa na mwana


.
Quran 6 : 101 Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi. Inamkinikaje Awe na mwana, hali Hana mke. Naye ndiye aliyeumba kila kitu (siyo baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu.

Inakuwa mjuzi wa kila kitu au muweza wa vyote ASHINDWE NA KITU KIMOJA TU!!! YAANA KUTO KUWA NA MWA A eti mpaka awe na mke?


Hapa unapata picha kuwa walitumwa na Miungu tofauti. Huhitaji kuvaa miwani ili ulione vizuri au ulielewe vyema.

👇👇👇👇
Quran 18:4-5


4. Na kiwaonye wale wanaosema Mwenyezi Mungu amejifanyia mtoto.

5. Wao hawana ilimu juu ya (jambo) hili wala baba zao ( hawana ujuzi juu ya jambo hili ilawanajisemea tu). Ni neno kubwa hilolitokalo katika vinywa vyao. Hawasemi ila uwongo tu.


Hapo ndio tupate kujua mbivu na mbichi.

Inamaana kuwa YESU ALIPOJIITA MWANA WA MUNG, alikosea na quran imekuja kupitia Muhammad imekuja kumuonya mtu ambaye hana kosa wala hakuwahi kutenda dhambi.


Kwa kauli ya Allah ya Muhammad mtume wake tunapata jibu kuwa YESU ni mwenye dhambi?

Haitokuwa hata siku kupata kosa la Yesu ila kujilisha upepo tu kewa Muhammad na mungu wake Allah.


Sasa twende kwenye utata huu ni kweli aliyejiita MWANA WA MUNGU ( ikaonekana ni kosa )  baadae aitwe MWENYE HEAHIMA MBINGUNI NA DUNIANI?

Quran 3:39

39. Mara Malaika akamlingania, hali amesima akisali chumbani, kwamba Mwenyezi Mungu anakupa khabari njema za (kuwa utazaa mtoto; umwite Yahya, atakaye kuwa mwenye kumsadikisha (Mtume atakayezaliwa)  kwa Nenolitokalo kwa Mwenyezi Mungu (Naye ni Nabii Isa) na  atakayekuwa Bwana kabisa na mtawa na nabii anayetokana na watu wema. (Naye ni nyinyi)


Aya hii inahusu kuzaliwa kwa YOHANA NA YESU. 


Kwanza Yohana atazaliwa na atatabiri kuhusu Ujio wa Yesu, na ya kuwa Yesu atakuwa Bwana.
Tafsiri ya BARWAN inasema MHEAHIMIWA MBINGUNI NA AKHERA.


Ni kweli huyu ATAKAYEKUWA MHESHIMIWA ndiye aliyejiita MWANA WA MUNGU?



Kwa kauli hii unapata picha kuwa Walitumwa na Miungu tofauti.


Kauli ya mwisho ya YESU NI HII


17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu (YOHANA 20:17)




MUNGU NI BABA YAKE, PIA NI BABA YETU. Huo ndio ukweli.

HUO NDIO UKWELI.

Aliyemtuma  YESU ni Tofauti na aliyemtuma Muhammad.


Huo ndio utofauti wao.
Mmoja ana mwana mwingine hana.



KAULI YA WA KWANZA HAIWEZI kupingwa baada ya miaka 600




TAMBUA KUWA ALIYEMTUMA YESU ANAKUBALI KUITWA BABA, Hii ni tofauti na aliyemtuma Muhammad.

Jumamosi, 25 Machi 2017

SUALA ZIMA ZA USHOGA KIBIBLIA

SUALA ZIMA LA USHOGA (MWANAUME KUOLEWA AU KUMUOA MWANAUME MWENZIWE)

Ni jambo ambalo ni chukizo kubwa sana mbele za MUNGU BABA, na mbele za Mwana-kondoo pamoja na Malaika WATAKATIFU wote. Wakati wa Ibrahimu na LUTU, MUNGU aliamua kuichoma Miji miwili, SODOMA NA GOMORA. kwa sababu ya dhambi hiyo 👇

Mwanzo 19: 12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa;

13 maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za BWANA; naye BWANA ametupeleka tupaharibu.

MUNGU hakuishia tu kuwaangamiza watu wa SODOMA na GOMORA, walioendekeza vitendo vya UFIRAJI na ULAWITI! hata wakati wa MUSA, Mungu aliweka sheria hiyo hiyo ya KIFO kwa watu wanaojihusisha na mapenzi ya JINSIA moja. 👇

Walawi 18:22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo.

Walawi 20:13 Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.

Suala zima la USHOGA, ni dhambi mbaya ambayo adhabu yake ni KIFO! haikuwa na msamaha kama ulivyo UONGO, uzushi, Ufisadi. Wahusika hawakupewa nafasi ya kutubia dhambi zao, hata kama wamefanya pasina kujua kuwa ni MACHUKIZO mbele za MUNGU! maana watu wa SODOMA na GOMORA hawakuwa wamepewa sheria ya kuwakataza kufanya kitendo hicho, lakini waliweza kuangamizwa! Kanisa LEO lipo kimya kabisa, na halichukui hatua yo yote kwa Wahuni wanaofungua makanisa kisha kufungisha ndoa za JINSIA hiyo, kitendo Ambacho kinatafsiriwa na wasiokuwa Wakristo kuwa, ni Halali KUFUNGISHWA ndoa hizo katika makanisa, na ukimya wa VIONGOZI wakubwa, ndiyo sababu ya Vitendo hivyo kushamiri, na kuendelea kuliharibia SIFA kanisa la MUNGU! japo maandiko yanasema 👇

Warumi 1:26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;

27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.

28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

Haina maana kwamba, MUNGU ameruhusu, la hasha! bali aliwaacha wayafanye hayo kisha wakapata malipo yaliyowastahili ambayo ni Mauti! Mungu hakutoa kibali hicho, kitendo cha KANISA, kukaa tu na kuwaacha Wahuni hao waendelee kujenga makanisa na kisha kufungisha ndoa za JINSIA MOJA ni dhahiri kuwa KANISA linakubaliana na Wahuni, maandiko yanasema. 👇

Warumi 1:32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.

Maandiko yanasema, hao wayatendayo hayo, kwa hukumu ya MUNGU ambayo ni ya haki wamestahili mauti, siyo tu wanaojihusisha na VITENDO hivyo, bali hata na wale wanaokubaliana navyo! nao pia wamestahili mauti. Kukubaliana navyo siyo lazima uifungishe ndoa hiyo, hata kitendo cha Kuwaacha wayatumie Makanisa na hatua ya kuwazuia haichukuliwi, basi ni kitendo cha kukubaliana nacho! na imekuwa ni machukizo kwa MUNGU, hata kuzififisha nguvu za KANISA, Yesu alipoona Hekalu limegeuzwa kuwa PANGO LA WAFANYA BIASHARA, alichukua hatua. 👇

Yohana 2:13 Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu.

14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng'ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi.

15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng'ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao;

16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara.

17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa nyumba yako utanila.

Sisi LEO ujasiri huu wa YESU KRISTO, tunashindwaje kuwa nao? tunashindwaje kupindua madhabahu zao wafungishao ndoa za JINSIA moja? Paulo alipoona KANISA LA KORINTHO limeanza kuingiza mambo ambayo hayastahili kuwamo ndani ya Kanisa, alichukua hatua ya kuwakemea, kuwa Mkusanyiko waoABEL SULEIMAN SHILIWA:
siyo wa WAFAIDA bali kwa hasara. 👇

1 Korintho 11:16 Lakini mtu ye yote akitaka kuleta fitina, sisi hatuna desturi kama hiyo, wala makanisa ya Mungu.

17 Lakini katika kuagiza haya, siwasifu, ya kwamba mnakusanyika, si kwa faida bali kwa hasara.

18 Kwa maana kwanza mkutanikapo kanisani nasikia kuna faraka kwenu; nami nusu nasadiki;

19 kwa maana lazima kuwapo na uzushi kwenu, ili waliokubaliwa wawe dhahiri kwenu.

20 Basi mkutanikapo pamoja haiwezekani kula chakula cha Bwana;

21 kwa maana kila mmoja hutangulia kutwaa chakula chake katika kule kula; hata huyu ana njaa, na huyu amelewa.

22 Je! Hamna nyumba za kulia na kunywea? Au mnalidharau kanisa la Mungu, na kuwatahayarisha hao wasio na kitu? Niwaambieni? Niwasifu? La! Siwasifu kwa ajili ya hayo.

Hata kama unaamini kuwa wewe haushi CHINI ya sheria, bado siyo sababu ya kukaa kimya! Kwani hao ambao wanafanya hayo, sheria bado inawahusu. 👇

1 TIMOTHEO 1:8 Lakini twajua ya kuwa sheria ni njema, kama mtu akiitumia kwa njia iliyo halali;

9 akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu wa haki, bali waasi, na wasio wataratibu, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji,

10 na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na likiwapo neno lo lote linginelo lisilopatana na mafundisho yenye uzima;

HAO WATU NI LAZIMA WASHUGHULIKIWE KWA SABABU SHERIA INAWAHUSU WAO, WEWE AMBAYE HUFANYI HAYO, UHUSIKI KATIKA SHERIA. KANISA LIAMKE.

Asanteni Wote mliosoma post hii

Mungu awabariki

Ijumaa, 17 Machi 2017

BWANA YESU ANAWATAFUTA WALIO WAKE Waihubiri INJILI

Bwana YESU anawatafuta watu walio waaminifu  ili waipeleke injili yake.
Anawatafute wateule wanaojua wajibu wao, majukumu yao na wito wao.
Ndugu, inakuaje unapenda kusifiwa na bosi wako kazini lakini hutaki kusifiwa na Bwana YESU aliyekupa injili yake ili uipeleke kwa watu wote?
Wewe hutaki kuipeleka injili, uko busy tu na kazi yako yenye malipo duniani tu na sio mbinguni.
Ndugu peleka injili ya KRISTO mbele, peleka injili kwa kuhubiri watu. Kama huna muda wa kuhubiri basi ipeleke injili kwa pesa yako kwa kuwasapoti wanaoipeleka injili. Peleka injili hata kwa kusambaza vipeperushi vya Neno la MUNGU, peleka injili hata kwa kuwaalika watu kwenda kwenye mikutano ya injili na ibadani kanisani, ni jukumu lako kuipeleka injili, ndugu timiza jukumu lako.
Kuna faida katika kumwamini YESU KRISTO na kulitii Neno la MUNGU.

Faida baadhi za kumwamini YESU na kulitii neno lake ni:

1.  Kuwa pamoja na KRISTO.
Mathayo 28:19-20 " Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la BABA, na MWANA, na ROHO MTAKATIFU ; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari."

2.  Kutenda mema.
2 Timotheo 3:16-17 " Kila andiko, lenye pumzi ya MUNGU, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;  ili mtu wa MUNGU awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema."

3.  Kushiriki pendo la MUNGU baada ya kumaliza kazi duniani.
Yohana 3:16 " Kwa maana jinsi hii MUNGU aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

Ndugu yangu nakuomba sana ihubiri injili ya KRISTO siku zote, huku ukiishi maisha matakatifu katika yeye na huku ukimtii ROHO MTAKATIFU.
MUNGU akubariki sana.