Ijumaa, 3 Machi 2017

JE UFALME WA MUNGU NI WA WATOTO TU NA SI WATU WAZIMA?

Karibu ndugu msomaji UNG'AMUE kitu.

UFALME WA MUNGU NI WA WATOTO WACHANGA  SI WATU WAZIMA!!!!!!!

BWAN ASIFIWE

Nakusalimu mtu wa MUNGU usishangae hicho kichwa cha somo nataka nikueleze jambo hili kidogo utanielewa namaanisha nn napokuambia ufalme wa MUNGU ni watoto wadogo si watu wazima ninamaanisha kweli unazijua sifa za mtoto Mdogo?

Sifa za mtoto Mdogo
=> mpole,mnyenyekevu,Hana makuu,si muongeaji,mtii,mkimya,ni mjinga katika ulimwengu huu,hajui dhambi,hana kiburi,dharau,majivuno,anaishi kutokana na maagizo ya wazazi wake.

Hizo ni baadhi tuu ya sifa za mtoto Mdogo je Ndugu yangu we ni mtoto mdogo?

Luka 18:15-17
15 Wakamletea na watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi walipoona waliwakemea.
16 Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao.
17 Amin, nawaambia, Mtu ye yote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.

Watu wenye mfano wa mtoto Mdogo ndio pekee wataiyona mbingu Ndugu yangu watu wengi hawana tabia za watoto wadogo ufalme wa MUNGU upookee kama mtoto Mdogo kwa sifa hizo hapo juu nilizoziolodhesha MUNGU wetu hupenda sna watu wenye tabia za watoto wadogo MUNGU alipendezwa na daudi hata alivyokuwa mkubwa japo kwa makosa yote aliyofanya bado Tabia ya utoto mbele za MUNGU haikutoka kwake

Mathayo 18:1-4
1 Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,
2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,
3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

Unaona aliyemkuu katika ufalme wa MUNGU?ni mtoto Mdogo na unatakiwa uongoke uwe kama mtoto Mdogo bila hivyo Mbinguni utapasikia unatakiwa kujinyenyekeshaye mbele za MUNGU ukiwa na sifa za mtoto huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni MUNGU hawafunulii watu wazima waliojawa kiburi dharau majivuno mashindano Bali watoto wachanga

Luka 10;21
21 Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza.

MUNGU amewaficha wenye hekima na akili (watu wazima) Bali amewafunulia watoto wachanga maana ndivyo MUNGU wetu apendavyo watu watu wanaomba MUNGU awafunulie mambo wanataka wazijue siri za MUNGU katika dunia hii wengine wanaomba MUNGU afunue macho yao waone sikiliza mtu wa MUNGU je ww unakifua cha kuhifadhi siri zake? We sio mtu wa lopo lopo muongeajei? Je wewe sio mpole na mtulivu?je ww ni mkimya kama mtoto mchanga mpaka akufunulie siri zake uwone?

Sikiliza MUNGU hashei siri zake wapumbavu watu wazima ung'ang'ania MUNGU nionesha nataka nione je unatabia za mtoto mchanga? Maana MUNGU hupenda kuwafunulia watoto wachanga ndivyo apendavyo yeye MUNGU hashei siri zake na watu wazima wapumbavu sikuambii uwe mtoto katika akili zako sivyo

1korinto 14:20
20 Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima.

Ndio usiwe mtoto katika akili zako lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga Bali katika akili zenu mkawe watu wazima ndivyo unavyotakiwa katika uovu wa namna yoyote kuwa mtoto usiwe muongeji usiwe na kiburi dharau majivuno mzinzi muasherati muongo msengenyaji maovu yoyote yale kwako uwe kama mtoto mchanga maana haya hayajui yeye mtoto mchanga Hapo ndipo MUNGU atakufunulia mengi na ufalme wa MUNGU utakaa ndani yako

Na MUNGU akubariki .

DHAMBI YA KUMKOSOA MWENYEZI MUNGU

<(") HII DHAMBI YA KUMKOSOA MUNGU NA UUMBAJI WAKE, JE NANI ATAPONA???
_________________________________
Ilikua  imezoeleka kuona  ni wasichana  na wanawake kujichubua ngozi zao,  ingawa  sio sahihi na wala si mpango wa Mungu  lakini  roho  hiyo  ya  mwanamke  Yezebeli  imepamba moto ktk nyakati hz  za  kumalizia,
na  sasa  imekuwa  kama  mchezo tu,  si wanawake, si wanaume tena  siku  hz  mpaka  na WACHUNGAJI nao wameingia ktk mtego huu wa Ibilisi,  nao  wamekua wakosoaji wakubwa wa Mungu na uumbaji wake.
_________________________________
Katika kusumbuka kuutafuta uzuri,  watu wengi leo  wanamtenda Mungu  dhambi  kwa  kumsahihisha,  kana kwamba  Mungu aliwaumbia viungo vyao kimakosa (kwamba  alikosea kuwaumba walivyo na badala yake angewaumba kama jinsi wanavyotaka wao),
*************************-***-****
Hii  si  sawa  hata  kidogo,  na ingawa  Mungu amenyamaza  lkn  ipo  siku ambayo  watu watajuta wakitafuta njia ya kutubu na wasiipate,
*********************************
Mungu anasema  kila alichokiumba na tazama kilikua chema (kikiwa kama kilivyo ktk asili yake) MWANZO 1:31.
_________________________________
Suala  la  kuvaa  nywele  za wafu (mawigi), kuweka  kucha  bandia,  kope, nyusi, meno na  hata kubadili asili ya ngozi kwa  kujichubua,  nakuambia  ipo  siku  inakuja ambayo watu  watajuta  kuvifanya,  na  siku  hiyo  haitawaonea  huruma  wachungaji wala  mama wachungaji wanaomtukana  Mungu  kwa  kumwona  hajui  kuumba  ila wao ndo  waumbaji wazuri  kuliko yeye,  maandiko yanasema,  Mtu  akimuheshimu  Mungu, Mungu pia atamuheshimu mtu huyo,  la   hakumuheshimu  basi  atahesabiwa kuwa ni mkosa, (1SAMWELI 2:30)
_______________________________
MAANDIKO  YAFUATAYO  YAKUSAIDIE KUELEWA VIZURI  UJUMBE HUU:
WARUMI 9:19-21,
ISAYA 29:16,
YEREMIA 13:23,
____ MWENYE MASIKIO NA ASIKIE______.


Ni kosa kubwa sana kumkosoa MWENYEZI MUNGU.

ALIPOUMBA VITU VYO VILIKUWA KAMILIFU VISIVYO NA KOSORO, je wewe ndio mjuzi kuliko YEYE?

TAFAKARI CHUKUA HATUA

KWA NINI NINAITEGEMEA DAMU NA JINA LA YESU?

Kinacho sababisha niitegemee DAMU NA JINA LA YESU NI KWA SABABU NILINUNULIWA NA YESU MWENYEWE KWA DAMU YAKE. NA NINAPATA MSAMAHA WA DHAMBI KWA JINA LAKE na ninasafishwa kwa DAMU YA YESU.

UFUNUO 5

9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,
10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.
11 Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,
12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.
13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele.
14 Na wale wenye uhai wanne wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka, wakasujudu.

BARAKA ZOTE, ZINAPATIKANA KWA JINA LA YESU,
MSAMAHA KWA JINA NA DAMU YA YESU.
TUNASAFISHWA KWA DAMU YA YESU NA KWA JINA LA YESU MWENYEWE.

NAJIVUNIA HILO katika Kumwamini.

Usiufanye moyo wako kuwa mgumu, jinyenyekeze KWA YESU NA utasamehewa na kuwa safi kwa DAMU NA JINA LAKE.

MUNGU AKUBARIKI .

Alhamisi, 2 Machi 2017

KUNA FAIDA KUBWA KATIKA KUTOA KULIKO KUPOKEA

KUNA FAIDA KUBWA ZAIDI KATIKA KUTOA KULIKO KATIKA KUPOKEA.

Shalom mteule wa KRISTO upendwaye sana na MUNGU BABA.

Karibu tujifunze Neno la MUNGU.

Matendo 20:35 ''Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana YESU, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.''

Ukitoa utasababisha aliyepokea amshukuru MUNGU na jambo hilo kukuongezea kitu wewe mtoaji maana wewe ndio chanzo cha shukrani hiyo.

Utoaji wako utakupa sifa na heshima.

Lakini pia ukitaka kuwa mtoaji anayetoa katika mpango wa MUNGU basi Fanyika kwanza wewe kuwa sadaka ndipo utoe sadaka.
Ukifanya hivyo utabarikiwa sana rohoni na mwilini.

''Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake MUNGU , itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza MUNGU , ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya MUNGU yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu. ''

Jambo muhimu pia la kukumbuka ni kwamba MUNGU hataki matoleo ya ubatili.
Matoleo ya ubatili ni sadaka isiyo sahihi mfano huwezi kuiba pesa harafu ukasema ''ngoja niipeleke kanisani ili MUNGU anibariki zaidi''. Hapo utakuwa unajidanganya wewe mwenyewe na huo ni ubatili mkubwa. Matoleo ya ubatili ni pamoja na kupeleka sadaka isiyo sahihi mfano una laki 1 mfukoni lakini unamtoleaMUNGU Tsh. 100. hii sio haki na kumbuka kwamba hata hiyo laki moja uliyonayo ni MUNGU kakupa na MUNGU hapa anaangalia tu utii wetu sio kwamba ana shida na pesa.

Lakini utoaji wa sadaka safi ni zaka kamili ni muhimu sana na ni agizo la MUNGU kwetu lenye matokeo mazuri sana kwetu watoaji.

Biblia inasema kwamba ni heri kutoa kuliko kupokea.
Maana yake nini?

Kuna faida kubwa zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.

FAIDA NNE(4) ZA KUTOA MATOLEO SAHIHI KWA MUNGU.

1. Ukitoa utakuwa unaweka hazina mbinguni ambapo hakuna atakayeiondoa.

Mathayo 6:19-21 '' Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.''

-Kutoa matoleo sahihi ni kuweka hazina mbinguni.

Hazina ni nini?

Hazina ni ni mali au vitu vya thamani  vinavyohifadhiwa eneo zuri kwa ajili ya matumizi ya baadae.

Kwa serikali, hazina ni mahali ambapo shughuli za serikali zinazohusu fedha zinaendeshwa.

Kiroho tunaweza kusema kwamba hazina ya wateule wa MUNGU ni mahali mbinguni ambapo matokeo ya utoaji wa mteule huonekana na kufanyiwa kazi yenye manufaa sasa kwa mteule huyo na baadae kwenye uzima wa milele.

Wako Malaika wa MUNGU walio katika kitengo cha uhazini mbinguni kiasi kwamba hakuna hazina ya mteule inayoweza kupotea wala kuibiwa wala kuondolewa.

Mhazini ni mtunza fedha au mali katika eneo zuri na salama, mbinguni wako Malaika katika eneo hilo hivyo Mteule unapotoa kwa moyo na kwa upendo kwa MUNGU hakika hazina yako mbinguni inaongezeka, ndio maana Biblia imesema kwamba ni heri kutoa kuliko kupokea.

Kuna faida kubwa katika kutoa kuliko katika kupokea.

Roho yako itakapokuwapo katika ufalme Wa MUNGU ndipo na hazina yako ya utoaji wako itakapokuwa.

2. Kitendo cha wewe kutoa maana yake unamjaribu MUNGU ili akukuze zaidi.

Malaki 3:10-12 ''Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema BWANA wa majeshi. Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema BWANA wa majeshi.''

Kuna watu shetani huwapangia magonjwa mara kwa mara lakini hawaumwi kwa sababu MUNGU anamkemea mharibifu wa afya zao kwa sababu tu ya utoaji wao sahihi na kwa uaminifu na upendo wa fungu la kumi na sadaka.

MUNGU anataka tumjaribu kwa matoleo.

MUNGU ameahidi madirisha ya mbinguni kufunguka. Madirisha ya mbinguni yakifunguka kwako kwa sababu ya utoaji wako sahihi na wa kudumu hakika huko mbinguni zitatoka baraka nyingi na upendeleo katika kazi, uchumba, ndoa na chochote kinachokuhusu.

MUNGU anaposema atakubariki kwa sababu ya uaminifu wako sio kwamba atakubariki pesa tu bali ni mambo mengi ya kukubariki.

Mwanzoni mwa maisha yangu ya wokovu nilikuwa na ugumu wa kutoa fungu la kumi lakini katika miezi ambayo sikuzingatia kutoa fungu la kumi nilikutana na matatizo ambayo nilitumia pesa mara tatu hadi saba zaidi ya fungu la kumi ambalo nilitakiwa kutoa.

MUNGU anaposema kwamba atamkemea yeye alaye uchumi wako hakika atamkemea.

Hata kama ni magonjwa ya mlipuko kitaifa lakini wewe mtoaji mwaminifu utashangaa tu uko salama, hapo MUNGU amemkemea anayetaka kukuharibia.

Mama mmoja alienda kwa mganga wa kienyeji na kupewa dawa ili kumpata baba mmoja aliyeokoka ambaye alikuwa mwaminifu kwa MUNGU, Yule dada alipewa nyoka ili nyoka yule amtume kwa yule kaka ili yule kaka amchukuie mkewe na kwa njia hiyo ampende yule dada wa nje. Yule dada akiwa na nyoka wake aliikaribia nyumba ya yule kaka na akamtuma yule nyoka ili akafanye mambo kwenye nyumba ile. Yule nyoka alienda na kurudi haraka akiwa amejeruhiwa na alipofika alimwuma yule aliyemtuma kisha akatokomea kusiko julikana. Wale watu wa MUNGU wala hawakumuona yule nyoka katika familia yao lakini yule dada aliteseka sana na hadi akaenda kwa mganga na mganga akaanza kumwambia hana dawa ya kumtibu huku akimtukana. Hakika MUNGU humkemea mharibifu katika mazingira ambayo sisi hatujui, ila uaminifu wetu kwa MUNGU katika utoaji wa zaka na saka hakika MUNGU hutuzingira.

Ukweli ni kwamba hakuna aliye mwaminifu hata mmoja ambaye akimtolea MUNGU habarikiwi, bali wote hubarikiwa katika maeneo mbalimbali katika maisha yao.

Hakika kuna faida nyingi sana katika utoaji.

3. Utoaji wako utakuwa sababisho la wewe kupata kitu fulani kutoka kwa MUNGU.

Mwanzo 8:16-22 '' Toka katika safina, wewe, na mkeo, na wanao, na wake za wanao pamoja nawe. Utoe pamoja nawe kila kilicho hai kilichomo pamoja nawe, chenye mwili, ndege, na mnyama, na kila kitambaacho, chenye kutambaa juu ya nchi; wajae katika nchi, wawe na uzazi, wakaongezeke katika nchi. Basi Nuhu akatoka, yeye, na wanawe, na mkewe, na wake za wanawe pamoja naye; kila mnyama, na kila kitambaacho, na kila ndege, kila kinachokwenda juu ya nchi kwa kabila zao, wakatoka katika safina. Nuhu akamjengea BWANA madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. BWANA akasikia harufu ya kumridhisha; BWANA akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya. Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma. ''

Baada tu ya Nuhu kutoka ndani ya safina alimjengea MUNGU Madhabahu kisha akatoa sadaka nzuri kwa MUNGU.

MUNGU baada tu ya kuikubali sadaka ya Nuhu alitoa baraka.

MUNGU alisema  Hatailaani nchi  wala kuipiga kwa gharika dunia yote, Hiyo ni baraka ya MUNGU inayodumu hata leo kwa sababu ya sadaka za Nuhu. Hata iweje leo haiwezekani dunia nzima kuzama kwenye maji kama ilivyotokea wakati wa Nuhu, hiyo ni baraka kwa Nuhu na uzao wake wote ambao ni mimi na wewe.

  MUNGU akiikubali sadaka yako hakika tarajia Muujiza wa MUNGU maishani mwako.

Kuna njia nyingi za MUNGU kukubariki kama utazingatia utoaji wa sadaka safi na zaka sahihi.

Sadaka inaweza ikafufua yale yaliyo kufa maishani mwako.

Dorkasi alikufa lakini sadaka zake zikawa muujiza wa kumfufua.

Hata leo yako mambo yaliyokufa maishani mwako lakini sadaka yako inaweza kuyafufua.

Utoaji wako unaweza kuzifufua baraka zako zilizokuwa zimekufa.

Hebu jifunze katika maandiko haya.

Matendo 9:36-41 '' Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa. Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani.  Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu. Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao. Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi.  Akampa mkono, akamwinua; hata akiisha kuwaita wale watakatifu na wajane akamweka mbele yao, hali yu hai. ''

4. Sadaka yako itakuwa ukumbusho mbele MUNGU.

Matendo  10:1-8 '' Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,  mtu mtauwa, mchaji wa MUNGU, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba MUNGU daima. Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa MUNGU, akimjia na kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za MUNGU. Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro. Yeye ni mgeni wa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi, ambaye nyumba yake iko pwani, atakuambia yakupasayo kutenda.  Na yule malaika aliyesema naye akiisha kuondoka, Kornelio akawaita wawili katika watumishi wake wa nyumbani, na askari mmoja, mtu mtauwa katika wale waliomhudumia daima; na alipokwisha kuwaeleza mambo yote akawatuma kwenda Yafa.''

Sadaka ya Kornelio ikawa ukumbusho kwa MUNGU.

Kuwa ukumbusho sio jambo dogo, Malaika alishuka kwa Kornelio kwa sababu ya utoaji wake sahihi wa matoleo kwa MUNGU.

Ni neema ya MUNGU malaika aje kwako ametumwa na MUNGU.

sadaka sahihi inaweza kumfanya MUNGU amtume Malaika.

Malaika wa MUNGU akishuka kwako ni kwa kusudi la MUNGU.

Sadaka kuwa ukumbusho kwa MUNGU ni jambo la muhimu sana.

Naamini kuanzia sasa utakuwa mwaminifu kwa MUNGU katika kutoa zaka kamili na sadaka halisi ili MUNGU akutendea Mema aliyoyakusudia maishani mwako.

Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.

MUNGU AKUBARIKI SANA.

UVIVU WA KUSOMA NENO LA MUNGU NDIO UMELETA MAJANGA HAYA!!!!

UVIVU WA KUSOMA NENO LA MUNGU NDIO UMELETA MAJIBU HAYA YA WAKRISTO WA SASA KATIKA HOJA ZIFUATAZO..* 👇👇

1⃣ *KUVAA NGUO ZA NUSU UCHI. (1 Timotheo 2 :9).*

_Mungu anaangalia Roho na si Nje._

2⃣ *KUIMBA NYIMBO ZA BONGOFLEVA (1 Petro 4 :2-4, Yakobo 4: 4)*

_Mi nasikiliza Ujumbe Tu, acha Ushamba nani amekuambia kuwa ni dhambi._

3⃣ *WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KUSHINDANISHWA (Efeso 4:11-12, 1 Wakorintho sura ya 12)*

_Kuna ubaya gani? Tunawatia Moyo._

4⃣ *WANA NDOA KUACHANA (Mathayo 19 :9)*

_Ruksa..! Ndoa imenishinda. Raha JIPE mwenyewe._

5⃣ *KUZINI (1 Wakorintho 6 :18)*

_Tutatubu._

6⃣ *WACHUNGAJI KUTAKA PESA NDIO WATOE HUDUMA (Mathayo 10 :9)*

_Unataka nile wapi? Mtenda Kazi ana stahili Ujira wake au umeshau mtendakazi wa madhabahuni hula vya madhabahuni._

7⃣ *KUFUNGA NA KUOMBA (Mathayo 26 :41,I Petro 4 :7).*

_Kuna haja gani ya kufunga wakati Nabii yupo? Vitambaa, Sabuni, mafuta ya UPAKO yapo?_

8⃣ *KUSOMA NENO (Kolosai 3:16)*.

_Yaan nakosa muda jamani, mmh basi TU Mungu mwenyewe anajua._

Wakat muda wote yupo online kwenye mitandao ya kijamii akichat na kupost picha.

9⃣ *KUHUDHURIA IBADANI (Waebarania 10 :25)*

_Nipo Busy sana, hizi Kazi nazo zinabana kweli_

🔟 *KUKEMEA DHAMBI (1 Timotheo 5 :20)*

_Hizo ni injili za zamani. Wewe TUTABIRIE tu na utufanyie Maombezi._

🔹🔹🔹🔹🔹🔹🔹

*JE, TUTAPATAJE KUPONA TUSIPOUJARI WOKOVU MKUU NAMNA HII* ❓

👉 *_lakini mwenye kuvumilia mpaka MWISHO ndio atakayeokoka_* .

  _Mathayo 24 :13_

*MPENDWA KUWA MACHO*

THAMANI YA DAMU YA YESU

IJUE THAMANI YA DAMU YA YESU NA UITEGEMEE DAMU HIYO IKUPE UZIMA.


Na Mungu kwa kutupa kuiona siku ya leo, pia namshukuru Mungu kwa ajili yako pia kukupa uzima siku ya leo.
Najua hakuna asiyeijua damu ya Yesu, kila mmoja anaifahamu. Lakini neno la Mungu ni jipya kila siku.
THAMANI YA DAMU YA YESU NI NINI?
>Thamani yake ni kutununua.
Ufunuo 5:9 "..Ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa" 
Pesa ikipoteza THAMANI haina uwezo wa kununua vitu vya gharama, kwa hiyo, DAMU ZA WANYAMA hazikuwa na thamani kuwanunua wanadamu walioshikiliwa dhambi, ndyiyo maana Kuhani alipokuwa anakwenda mbele za Bwana na damu za wanyama dhambi zao hazikuondolewa bali zilifunikwa.Maandiko yanasema......"MAANA HAIWEZEKANI DAMU YA MAFAHARI NA MBUZI KUONDOA DHAMBI" Waebrania 10:4.
Maana yake ni nini anaposema,..."HAIWEZEKANI" ni kwa sababu thamani yake haitoshi. Ndiyo maana mwanadamu akashindwa kuñunuliwa akabaki chini ya kifungo cha dhambi, deni likabaki pale pale,.......... kama natania kasome biblia yako utaambiwa.."LAKINI KATIKA DHABIHU HIZO LIKO KUMBUKUMBU LA DHAMBI KILA MWAKA" Waebrania 10:4.
Mtu akikwambia"WEWE UNA DHAMBI" mwambie..."MIMI SIKO CHINI YA DENI LA DHAMBI" mimi sasa ni kanisa la Kristo nimenunuliwa kwa damu isiyopungua THAMANI yake maandiko yananiambia..."...Mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenywe" Mdo 20:28.
(A) DAMU YA YESU INAONDOA 
DHAMBI.
1 Yohana 1:9 "Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
(B) DAMU YA YESU INATUHESABABIA
HAKI.
Warumi 5:9 "Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye"
(C) DAMU YA YESU INATUPA UJASIRI
WA KWENDA MBELE ZA MUNGU.
Waebrania 10:19 "Basi, ndugu, kwa kuwa tunaujasiri wa kupangia patakatifu kwa damu ya Yesu".
MUNGU AKUBARIKI SANÀ.
KAMA HUJAOKOKA OKOKA SASA
MAANA BAADA YA KUFA NI HUKUMU
Waebrani 9:27.

Jumatano, 1 Machi 2017

KWA NINI BAADHI YA WAKRISTO WANASUMBULIWA NA NGUVU ZA GIZA HUKU WAMEOKOKA

Karibu katika mada hii ujifunze kitu, kuhusu MTU kuokoka ila akasumbuliwa na nguvu za Giza / uchawi.


Zajue sababu zinazo sababisha halo hiyo.


KWA NINI baadhi ya WAKRISTO WANASUMBULIWA NA WACHAWI ilhali WAMEMPOKEA Yesu KRISTO?
________________________________________
________________________________________.

Kuna sababu kama nne zinazosababisha.

1. Dhambi - ukiwa na dhambi hakuna kizuizi lazima mchawi atakusumbua maana uko mbali na MUNGU.

2. Woga - ukimuogopa mchawi lazima akusumbue. cha msingi kwako ni IMANI DHABITI KUWA uchawi si kitu kwako.

3. Ujinga - Hapa ni pale unapojua wazi fika kwamba mchawi hana mamlaka juu yako bado unaamini maneno ya walioshindwa na kukuogopesha unashindwa kujiamini.

4. KUDUMAA / KUTOKUKUA - Mpendwa usipokuwa katika KUMUAMINI MUNGU hakika umedumaa. hapo lazima wachawi wakusumbue maana Hujakua bado fikra zako ziko pale pale hujiongezi.

Ukijitenga na MUNGU imani yako huwa chini ya viwango yakupasa UAMINI KWELI KWELI uwe na IMANI YA DHATI.

USIYUMBISHWE NA LOLOTE.

naishia hapo kwa leo.


cha msingi ACHA DHAMBI , DUMU KATIKA KUOMBA, MTEGEMEE MUNGU hakika WACHAWI SI KITU kwako.


Mungu akubariki.