Ijumaa, 3 Machi 2017

JE UFALME WA MUNGU NI WA WATOTO TU NA SI WATU WAZIMA?

Karibu ndugu msomaji UNG'AMUE kitu.

UFALME WA MUNGU NI WA WATOTO WACHANGA  SI WATU WAZIMA!!!!!!!

BWAN ASIFIWE

Nakusalimu mtu wa MUNGU usishangae hicho kichwa cha somo nataka nikueleze jambo hili kidogo utanielewa namaanisha nn napokuambia ufalme wa MUNGU ni watoto wadogo si watu wazima ninamaanisha kweli unazijua sifa za mtoto Mdogo?

Sifa za mtoto Mdogo
=> mpole,mnyenyekevu,Hana makuu,si muongeaji,mtii,mkimya,ni mjinga katika ulimwengu huu,hajui dhambi,hana kiburi,dharau,majivuno,anaishi kutokana na maagizo ya wazazi wake.

Hizo ni baadhi tuu ya sifa za mtoto Mdogo je Ndugu yangu we ni mtoto mdogo?

Luka 18:15-17
15 Wakamletea na watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi walipoona waliwakemea.
16 Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao.
17 Amin, nawaambia, Mtu ye yote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.

Watu wenye mfano wa mtoto Mdogo ndio pekee wataiyona mbingu Ndugu yangu watu wengi hawana tabia za watoto wadogo ufalme wa MUNGU upookee kama mtoto Mdogo kwa sifa hizo hapo juu nilizoziolodhesha MUNGU wetu hupenda sna watu wenye tabia za watoto wadogo MUNGU alipendezwa na daudi hata alivyokuwa mkubwa japo kwa makosa yote aliyofanya bado Tabia ya utoto mbele za MUNGU haikutoka kwake

Mathayo 18:1-4
1 Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,
2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,
3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

Unaona aliyemkuu katika ufalme wa MUNGU?ni mtoto Mdogo na unatakiwa uongoke uwe kama mtoto Mdogo bila hivyo Mbinguni utapasikia unatakiwa kujinyenyekeshaye mbele za MUNGU ukiwa na sifa za mtoto huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni MUNGU hawafunulii watu wazima waliojawa kiburi dharau majivuno mashindano Bali watoto wachanga

Luka 10;21
21 Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza.

MUNGU amewaficha wenye hekima na akili (watu wazima) Bali amewafunulia watoto wachanga maana ndivyo MUNGU wetu apendavyo watu watu wanaomba MUNGU awafunulie mambo wanataka wazijue siri za MUNGU katika dunia hii wengine wanaomba MUNGU afunue macho yao waone sikiliza mtu wa MUNGU je ww unakifua cha kuhifadhi siri zake? We sio mtu wa lopo lopo muongeajei? Je wewe sio mpole na mtulivu?je ww ni mkimya kama mtoto mchanga mpaka akufunulie siri zake uwone?

Sikiliza MUNGU hashei siri zake wapumbavu watu wazima ung'ang'ania MUNGU nionesha nataka nione je unatabia za mtoto mchanga? Maana MUNGU hupenda kuwafunulia watoto wachanga ndivyo apendavyo yeye MUNGU hashei siri zake na watu wazima wapumbavu sikuambii uwe mtoto katika akili zako sivyo

1korinto 14:20
20 Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima.

Ndio usiwe mtoto katika akili zako lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga Bali katika akili zenu mkawe watu wazima ndivyo unavyotakiwa katika uovu wa namna yoyote kuwa mtoto usiwe muongeji usiwe na kiburi dharau majivuno mzinzi muasherati muongo msengenyaji maovu yoyote yale kwako uwe kama mtoto mchanga maana haya hayajui yeye mtoto mchanga Hapo ndipo MUNGU atakufunulia mengi na ufalme wa MUNGU utakaa ndani yako

Na MUNGU akubariki .

Maoni 1 :

  1. Hakika nimebarikiwa mtumishi maana nilikuwa najiuliza kwanini yesu ali wafananisha watoto wadogo na ufalme wa mbinguni basi leo nimepata jibu lililo nyooka. Asanteee sana

    JibuFuta