Ijumaa, 3 Machi 2017

DHAMBI YA KUMKOSOA MWENYEZI MUNGU

<(") HII DHAMBI YA KUMKOSOA MUNGU NA UUMBAJI WAKE, JE NANI ATAPONA???
_________________________________
Ilikua  imezoeleka kuona  ni wasichana  na wanawake kujichubua ngozi zao,  ingawa  sio sahihi na wala si mpango wa Mungu  lakini  roho  hiyo  ya  mwanamke  Yezebeli  imepamba moto ktk nyakati hz  za  kumalizia,
na  sasa  imekuwa  kama  mchezo tu,  si wanawake, si wanaume tena  siku  hz  mpaka  na WACHUNGAJI nao wameingia ktk mtego huu wa Ibilisi,  nao  wamekua wakosoaji wakubwa wa Mungu na uumbaji wake.
_________________________________
Katika kusumbuka kuutafuta uzuri,  watu wengi leo  wanamtenda Mungu  dhambi  kwa  kumsahihisha,  kana kwamba  Mungu aliwaumbia viungo vyao kimakosa (kwamba  alikosea kuwaumba walivyo na badala yake angewaumba kama jinsi wanavyotaka wao),
*************************-***-****
Hii  si  sawa  hata  kidogo,  na ingawa  Mungu amenyamaza  lkn  ipo  siku ambayo  watu watajuta wakitafuta njia ya kutubu na wasiipate,
*********************************
Mungu anasema  kila alichokiumba na tazama kilikua chema (kikiwa kama kilivyo ktk asili yake) MWANZO 1:31.
_________________________________
Suala  la  kuvaa  nywele  za wafu (mawigi), kuweka  kucha  bandia,  kope, nyusi, meno na  hata kubadili asili ya ngozi kwa  kujichubua,  nakuambia  ipo  siku  inakuja ambayo watu  watajuta  kuvifanya,  na  siku  hiyo  haitawaonea  huruma  wachungaji wala  mama wachungaji wanaomtukana  Mungu  kwa  kumwona  hajui  kuumba  ila wao ndo  waumbaji wazuri  kuliko yeye,  maandiko yanasema,  Mtu  akimuheshimu  Mungu, Mungu pia atamuheshimu mtu huyo,  la   hakumuheshimu  basi  atahesabiwa kuwa ni mkosa, (1SAMWELI 2:30)
_______________________________
MAANDIKO  YAFUATAYO  YAKUSAIDIE KUELEWA VIZURI  UJUMBE HUU:
WARUMI 9:19-21,
ISAYA 29:16,
YEREMIA 13:23,
____ MWENYE MASIKIO NA ASIKIE______.


Ni kosa kubwa sana kumkosoa MWENYEZI MUNGU.

ALIPOUMBA VITU VYO VILIKUWA KAMILIFU VISIVYO NA KOSORO, je wewe ndio mjuzi kuliko YEYE?

TAFAKARI CHUKUA HATUA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni