UVIVU WA KUSOMA NENO LA MUNGU NDIO UMELETA MAJIBU HAYA YA WAKRISTO WA SASA KATIKA HOJA ZIFUATAZO..* 👇👇
1⃣ *KUVAA NGUO ZA NUSU UCHI. (1 Timotheo 2 :9).*
_Mungu anaangalia Roho na si Nje._
2⃣ *KUIMBA NYIMBO ZA BONGOFLEVA (1 Petro 4 :2-4, Yakobo 4: 4)*
_Mi nasikiliza Ujumbe Tu, acha Ushamba nani amekuambia kuwa ni dhambi._
3⃣ *WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KUSHINDANISHWA (Efeso 4:11-12, 1 Wakorintho sura ya 12)*
_Kuna ubaya gani? Tunawatia Moyo._
4⃣ *WANA NDOA KUACHANA (Mathayo 19 :9)*
_Ruksa..! Ndoa imenishinda. Raha JIPE mwenyewe._
5⃣ *KUZINI (1 Wakorintho 6 :18)*
_Tutatubu._
6⃣ *WACHUNGAJI KUTAKA PESA NDIO WATOE HUDUMA (Mathayo 10 :9)*
_Unataka nile wapi? Mtenda Kazi ana stahili Ujira wake au umeshau mtendakazi wa madhabahuni hula vya madhabahuni._
7⃣ *KUFUNGA NA KUOMBA (Mathayo 26 :41,I Petro 4 :7).*
_Kuna haja gani ya kufunga wakati Nabii yupo? Vitambaa, Sabuni, mafuta ya UPAKO yapo?_
8⃣ *KUSOMA NENO (Kolosai 3:16)*.
_Yaan nakosa muda jamani, mmh basi TU Mungu mwenyewe anajua._
Wakat muda wote yupo online kwenye mitandao ya kijamii akichat na kupost picha.
9⃣ *KUHUDHURIA IBADANI (Waebarania 10 :25)*
_Nipo Busy sana, hizi Kazi nazo zinabana kweli_
🔟 *KUKEMEA DHAMBI (1 Timotheo 5 :20)*
_Hizo ni injili za zamani. Wewe TUTABIRIE tu na utufanyie Maombezi._
🔹🔹🔹🔹🔹🔹🔹
*JE, TUTAPATAJE KUPONA TUSIPOUJARI WOKOVU MKUU NAMNA HII* ❓
👉 *_lakini mwenye kuvumilia mpaka MWISHO ndio atakayeokoka_* .
_Mathayo 24 :13_
*MPENDWA KUWA MACHO*
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni