Alhamisi, 2 Machi 2017

UVIVU WA KUSOMA NENO LA MUNGU NDIO UMELETA MAJANGA HAYA!!!!

UVIVU WA KUSOMA NENO LA MUNGU NDIO UMELETA MAJIBU HAYA YA WAKRISTO WA SASA KATIKA HOJA ZIFUATAZO..* 👇👇

1⃣ *KUVAA NGUO ZA NUSU UCHI. (1 Timotheo 2 :9).*

_Mungu anaangalia Roho na si Nje._

2⃣ *KUIMBA NYIMBO ZA BONGOFLEVA (1 Petro 4 :2-4, Yakobo 4: 4)*

_Mi nasikiliza Ujumbe Tu, acha Ushamba nani amekuambia kuwa ni dhambi._

3⃣ *WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KUSHINDANISHWA (Efeso 4:11-12, 1 Wakorintho sura ya 12)*

_Kuna ubaya gani? Tunawatia Moyo._

4⃣ *WANA NDOA KUACHANA (Mathayo 19 :9)*

_Ruksa..! Ndoa imenishinda. Raha JIPE mwenyewe._

5⃣ *KUZINI (1 Wakorintho 6 :18)*

_Tutatubu._

6⃣ *WACHUNGAJI KUTAKA PESA NDIO WATOE HUDUMA (Mathayo 10 :9)*

_Unataka nile wapi? Mtenda Kazi ana stahili Ujira wake au umeshau mtendakazi wa madhabahuni hula vya madhabahuni._

7⃣ *KUFUNGA NA KUOMBA (Mathayo 26 :41,I Petro 4 :7).*

_Kuna haja gani ya kufunga wakati Nabii yupo? Vitambaa, Sabuni, mafuta ya UPAKO yapo?_

8⃣ *KUSOMA NENO (Kolosai 3:16)*.

_Yaan nakosa muda jamani, mmh basi TU Mungu mwenyewe anajua._

Wakat muda wote yupo online kwenye mitandao ya kijamii akichat na kupost picha.

9⃣ *KUHUDHURIA IBADANI (Waebarania 10 :25)*

_Nipo Busy sana, hizi Kazi nazo zinabana kweli_

🔟 *KUKEMEA DHAMBI (1 Timotheo 5 :20)*

_Hizo ni injili za zamani. Wewe TUTABIRIE tu na utufanyie Maombezi._

🔹🔹🔹🔹🔹🔹🔹

*JE, TUTAPATAJE KUPONA TUSIPOUJARI WOKOVU MKUU NAMNA HII* ❓

👉 *_lakini mwenye kuvumilia mpaka MWISHO ndio atakayeokoka_* .

  _Mathayo 24 :13_

*MPENDWA KUWA MACHO*

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni