Ijumaa, 3 Machi 2017

KWA NINI NINAITEGEMEA DAMU NA JINA LA YESU?

Kinacho sababisha niitegemee DAMU NA JINA LA YESU NI KWA SABABU NILINUNULIWA NA YESU MWENYEWE KWA DAMU YAKE. NA NINAPATA MSAMAHA WA DHAMBI KWA JINA LAKE na ninasafishwa kwa DAMU YA YESU.

UFUNUO 5

9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,
10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.
11 Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,
12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.
13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele.
14 Na wale wenye uhai wanne wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka, wakasujudu.

BARAKA ZOTE, ZINAPATIKANA KWA JINA LA YESU,
MSAMAHA KWA JINA NA DAMU YA YESU.
TUNASAFISHWA KWA DAMU YA YESU NA KWA JINA LA YESU MWENYEWE.

NAJIVUNIA HILO katika Kumwamini.

Usiufanye moyo wako kuwa mgumu, jinyenyekeze KWA YESU NA utasamehewa na kuwa safi kwa DAMU NA JINA LAKE.

MUNGU AKUBARIKI .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni